Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Requiem in Re minore, per coro maschile e orchestra
Ratiba Podcast
Papa Francisko katika sala. Papa Francisko katika sala.  

Papa Francisko katika sala kwenye Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu

Papa Francisko Jumamosi tarehe 12 Aprili 2025 alikwenda katika basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu ili kutoa heshima kwa Bikira Maria Afya ya Waroma,kabla ya kuanza Juma Kuu.Hayo yalielezwa na Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Vatican.

Vatican News

"Mapema alasiri ya leo, Papa Francisko alikwenda kwenye Basilika ya Mtakatifu  Maria Mkuu katika kesha la Dominika ya Matawi, na mwanzo wa Juma Kuu Takatifu, alikaa kitambo na kusali mbele ya picha ya Bikira, Salus Populi Romani, yaani Bikira  Afya ya Watu wa Roma." Hayo ndiyo yaliyoelezwa na Ofisi ya Vyombo vya Habari Vatican, alasiri  Jumamois tarehe 12 Aprili 2025.

Uhusiano wa Papa na Picha ya Bikira Salus Populi Romani

Uhusiano kati ya Papa Francisko  na  Picha ya Bikira Afya ya Watu wa Roma (Salus Populi Romani) umekuwa wa kimwana. Mwisho mwa kulazwa kwake hospitalini Gemelli, Roma majuma matatu yaliyopita, Papa alikuwa amesimama kwenye uwanja mbele ya Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu bila kuingia ndani, kabla ya kurejea makao yake, katika Nyumba ya Mtakatifu  Marta, ili kusali na kupeleka  shada la  maua liwekwe mbele ya Picha ya Bikira, alilokabidhi kwa Kardinali Rolandas Makrickas, Mkuu mwenza wa Basilika hiyo. Hilo ndilo lilikuwa ni shada la maua ya njano ambalo Bi. Carmela Mancuso alikuwa amempelekea Papa na baada ya Papa Francisko kutoa shukrani kwa umma kwa kumtambua katika umati wa watu alipokuwa juu ya ghorofa  katika hospitali ya Gemelli.

Desturi ya Papa tangu 2013

Heshima kwa picha  ya Maria Salus Populi Romani ni desturi ya Baba Mtakatifu Francisko iliyoanza tarehe 14 Machi 2013, siku moja baada ya kuchaguliwa kwake, na imedumishwa kabla na baada ya kila akifanya ziara za kitume  na kichungaji. Na hatimaye, kwenda kwake mnamo Machi 23,  ilikuwa kama kuashiria mwisho wa safari ya hospitali na mwanzo wa safari mpya ya kupata nafuu akiwa makazi yake katika nyumba ya Mtakatifu  Marta mjini Vatican.

Ziara ya Mwisho ya Kitume ya 47 huko Ajaccio, Corsica

Ziara ya mwisho katika Kanisa Kuu la  Kirumi  zaidi ya mia moja iliyofanyika, ilikuwa ni  tarehe 14 Desemba 2024 wakati Papa alipokwenda kusali kwa kuzingatia ziara yake ya kitume ya 47 ya kwenda huko Ajaccio, kisiwani Corsica, kwa ajili ya hitimisho la Kongamano la "La Religiosité Populaire en Mediterranée", yaani "Udini Maarufu wa watu wa Mediterranea."

Papa katika basilika ya Maria Mkuu

 

 

12 Aprili 2025, 17:04
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031