Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Requiem in Re minore, K626, per soli, coro e orchestra
Ratiba Podcast
Dominika 6 Aprili 2025 Papa aliwashangaza waamini katika Uwanja wa Mtakatifu Petro,tendo hili pia limerudia tarehe 10 Aprili katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro. Dominika 6 Aprili 2025 Papa aliwashangaza waamini katika Uwanja wa Mtakatifu Petro,tendo hili pia limerudia tarehe 10 Aprili katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Papa awashangaza waamini ndani ya Kanisa la Mtakatifu Petro akisali katika kaburi la Papa Pius X

Tokeo lingine lisiloratibiwa la Papa baada ya lile la Dominika iliyopita,akitokea katika makazi yake ya Mtakatifu Marta,mahali ambako anaendelea kupata nafuu na ameanzisha tena mikutano kadhaa.Papa alifika katika Basilika muda wa saa 7.00 mchana ambapo alikutana na mamia ya waamini waliokuwa na shauku kubwa waliofika kumsalimia na kubarikiwa naye.

Na Salvatore Cernuzio – Vatican.

Ilikuwa karibu saa 7:00 za mchana  katika Basilika ya Mtakatifu Petro wakati baadhi ya wanawake walisikika wakipaza sauti kwenye vinjia: "Papa yuko hapa! Papa yuko hapa!" Baada ya mshangao wa Dominika iliyopita, (Aprili 6), pale ambapo waamini elfu 20 walikuwa katika Uwanja wa Mtakatifu Petro, kwa ajili ya Jubilei ya Wagonjwa na ya Ulimwengu wa Kiafya kwa ghafla walipomwona Papa akiwasili kwenye kiti cha magurudumu, tukio hilo limerudiwa tena mchana wa Alhamisi tarehe 10 Aprili 2025,  wakati Papa Francisko alipendelea kutoka kidogo katika makazi yake ya Mtakatifu Marta, ambapo anaendelea na matibabu yake na kuvuka Mlango wa Maombi ili kwenda kwenye Basilika. Ilikuwa ni chini ya dakika kumi za sala ya kimya mbele ya kaburi la Papa Pius X, Papa ambaye amekuwa akisema  alikuwa karibu sana na Papa huyo na ambaye pia alikwenda kusali Dominika iliyopita.

Mamia wamsalimia Papa

Hata hivyo, dakika chache zilitosha kuwashtua mamia ya watu waliokuwa wamekuja kuhiji katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro walikusanyika kumsalimu Papa. Miongoni mwao walikuwa pia baadhi ya wasanii warejeshaji ambao walikuwa na shughuli nyingi wakati huo nyuma ya pazia kwa kazi za ndani zilizofanywa katika miezi ya hivi karibuni na  Kiwanda cha Mtakatifu Petro (Fabbrica di San Pietro,) ambao walipeana mikono na Jorge Mario Bergoglio, watoto kadhaa aliowabariki na makundi yote ya mahujaji walikuwa jijini  Roma kwa ajili ya Jubilei. "Hisia nyingi sana, maono yangu yalififia kutokana na machozi na sikuweza hata kupiga picha," Monsinyo Valerio Di Palma,Mwanasheria wa Kanisa la Mtakatifu Petro alielezea vyombo vya habari vya Vatican.Alikuwa amerudi kwenye sakrestia, karibu 6.50 mchana kwa hiyo, dakika kumi baadaye alitoka nje akivutiwa na msukosuko huo na kuona kiti cha magurudumu na Papa, kikisukumwa na Massimiliano Strappetti, msaidizi wa afya ya kibinafsi. Na Pande zote kulikuwa na walinzi wakijaribu kudumisha utulivu ndani ya Kanisa Kuu.

Baraka na salamu

“Papa alipitia Mlango wa Sala na kisha akaenda kwenye Madhabahu ya Kiti kitakatifu na hatimaye kwenye kaburi la Mtakatifu Pius X ili kusali. Mwishoni alisalimia watu wachache, kwa kadiri alivyoweza,” kwa maelezo ya  Monsinyo Di Palma.” Hakuna maneno kutoka kwa Papa Francisko, bali ishara tu. Ishara za ukaribu na upendo kwa wale aliowakuta mbele yake, wengine hata walijipanga ili kupata muda wa ukaribu na Askofu wa Roma katika wakati huu ambao, kutokana na kutoonekana hadharani kumekuwa nadra sana: "Kila mtu alikimbia akijua kuwa Papa amefika ghafla." Kadahalika "Papa Francisko  alijionesha kwa watu akiwa na blanketi ndogo  miguuni ili kumkinga na baridi na mirija za pua za  oksijeni: "Hii ilituchochea, kumuona hivi 'akiwa na nguo za kiraia', rahisi. Kila mtu alikuwa akilia, hata usalama. Watoto wengine walikwenda karibu na Papa, mwanamke alibarikiwa kwa machozi. Kwa sababu ni ishara kwamba amepona, ndiyo, anateseka lakini yuko karibu. Kilichonigusa ni macho yake: makubwa, angavu. Mtazamo huu wa kupenya na makini. Hakusema chochote: alisalimia na kubariki. Nilimwambia, Baba Mtakatifu, tunakusubiri mapema urudi hapa tena. Alitabasamu," alihitimisha.

Papa Francisko awashangaza waamini
10 Aprili 2025, 17:24
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031