Tafuta

Sr. Jane Wakahiu akizungumza na wale waliokusanyika katika Kongamano la Dunia la SIGNIS 2026 jijini Kigali,Rwanda. Sr. Jane Wakahiu akizungumza na wale waliokusanyika katika Kongamano la Dunia la SIGNIS 2026 jijini Kigali,Rwanda. 

Kupaza sauti za watawa Wakatoliki katika uwanja wa umma

Asubuhi ya tatu na ya mwisho ya Kongamano la Dunia la SIGNIS ililenga mchango muhimu wa watawa Wakatoliki kwa Kanisa na kwa jamii. Sr. Jane Wakahiu, PhD Msaidizi Makamu wa Rais wa Operesheni na Mkuu wa Programu, muko wa Watawa wakatoliki wa Conrad N. Hilton alitafakari uzoefu wake wa kuandamana na wanawake watawa duniani kote.

Na Angella Rwezaula,Sr Ernestina Patrick Lasway,Sr Michelle Njeri,Sr FrancineMarie Cooper - Kigali, Rwanda.

Watawa wakatoliki hawapaswi kuonekana katika nyanja ya umma. Kupitia mipango kama vile Mpango wa Pentekoste na Wito wa Hekima, Kanisa linawekeza katika mafunzo ya mawasiliano ili kuwasaidia watawa kushiriki historia zinazoibuka kutoka pembezoni mwa dunia. Kujitolea huku kwa kukuza sauti zao kulikuwa katikati ya asubuhi ya tatu na ya mwisho ya Kongamano la Dunia la SIGNIS, ambalo lililenga mchango muhimu wa watawa kwa Kanisa na jamii. Akihutubia washiriki, Sr. Jane Wakahiu, PhD, Makamu wa Rais Mshiriki wa Operesheni za Programu na Mkuu wa Mpango wa Masista Wakatoliki katika Mfuko wa Conrad N. Hilton, alitafakari uzoefu wake akifanya kazi na watawa kote ulimwenguni.

mawasiliano kama kitendo cha upendo ni njia ya kuunganisha, kufunza na kukuza sauti za watawa,
mawasiliano kama kitendo cha upendo ni njia ya kuunganisha, kufunza na kukuza sauti za watawa,

Akiwahutubia wawasilianaji katika Kongamano la Dunia la SIGNIS, mnamo tarehe 6 Agosti, 2026, Sr. Jane Wakahiu, alilenga miradi miwili: Mpango wa Pentekoste unaotekelezwa na Baraza la kipapa la mawasiliano - mpango wa kuunganisha, kufunza na kukuza sauti za watawa, na Wito wa Hekima, Mpango unaowaleta Watawa Wakatoliki pamoja na majukwaa ya vyombo vya habari vya kibiashara.

Ushahidi wa Kinabii

Katika uwasilishaji wake, kuhusu "Ushahidi wa Kinabii katika Kusimulia historia na Kukuza Sauti za Masista Wakatoliki katika Uwanja wa Umma," Sr Jane, alilenga mada tano: mawasiliano kama uhusiano wa Mungu na wanadamu, mawasiliano kama daraja, mawasiliano ya kutoa matumaini, mawasiliano ya kuwaweka wale walio pembezoni, na mawasiliano kama kitendo cha upendo.

Mungu kama chanzo cha mawasiliano

"Kupitia mipango ya Pentekoste na Wito wa Hekima, tumeitwa kusikiliza, na kutambua jinsi tunavyowasiliana," alisema. Akinukuu Biblia, na kusisitiza kwamba mawasiliano yana asili yake kwa Mungu tangu kuumbwa kwa ulimwengu: "Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu" (Yohana 1:1). "Kwa hivyo, mawasiliano si tu upitishaji wa habari. Yameunganishwa katika uhusiano wa Mungu na wanadamu. Huumba, hufunua, huita, na hutoa uzima," alisema.

Usimulizi wa Historia kama Huduma ya Injili

Sr. Jane alisema kwamba, kwa wale wanaoshiriki katika mawasiliano ya Kikatoliki, usimulizi wa historia si utangazaji tu. Ni kitendo cha huduma kwa Injili. "Inawasaidia watu kutambua uwepo wa Mungu duniani na inatukumbusha kwamba hata katika nyakati za migogoro, kutokuwa na uhakika, na mateso, neema inaendelea kufunuliwa kimya kimya, mara nyingi katika sehemu ambazo vichwa vya habari havifikiki," aliongeza.

Sr. Nina Krapić wakati wa uwasilishaji  kuhusu uwakilishi wa Watawa katika vyombo vya habari na kuhusu Mpango wa Pentekoste
Sr. Nina Krapić wakati wa uwasilishaji kuhusu uwakilishi wa Watawa katika vyombo vya habari na kuhusu Mpango wa Pentekoste

Kuandika upya simulizi kuhusu watawa

Akitafakari uwakilishi wa masista Wakatoliki katika vyombo vya habari, Sr. Nina Krapić, Naibu Mkurugenzi wa Ofisi ya Vyombo vya Habari ya Vatican, alitaka taswira halisi zaidi ya maisha ya watawa ambayo inazidi picha zinazosambaa mara nyingi kwenye mitandao ya kijamii. Ingawa maudhui mepesi yanaweza kuvutia umakini, alisema hayapaswi kupuuza ukweli wa utume wa masista wanapohudumu katika hospitali, shule, jamii za wakimbizi, na maeneo ya umaskini, wakiandamana na watu kupitia baadhi ya mapambano ya ndani kabisa ya maisha na furaha kubwa zaidi. Uwepo wao wa kila siku pembezoni, alibainisha, hutoa uzoefu mwingi na matumaini ambayo yanastahili kushirikiwa.

Sr. Nina pia aliwasilisha Mpango wa Pentekoste, juhudi inaounganisha mtandao wa kimataifa wa masista wanaohusika katika mawasiliano. Kupitia uundaji wa kitaaluma na uandishi wa habari shirikishi, mpango huo unawapa watawa uwezo wa kusimulia historia kutoka pembezoni pamoja na watu wanaowahudumia. Kwa kuimarisha sauti yao katika vyombo vya habari, alisema, mpango huo unalenga kufichua ushuhuda wa kudumu wa maisha ya kitawa na kuhamasisha mshikamano mkubwa zaidi na wale wanaohitaji zaidi.

Sr. Nina Krapić, Dkt. Peter Monthienvichienchai (Katibu Mkuu wa SIGNIS/Washiriki katika mradi wa 'Wisdom Calls' kutoka Afrika, Asia na Amerika ya Kusini), na Sr. Jane Wakahiu
Sr. Nina Krapić, Dkt. Peter Monthienvichienchai (Katibu Mkuu wa SIGNIS/Washiriki katika mradi wa 'Wisdom Calls' kutoka Afrika, Asia na Amerika ya Kusini), na Sr. Jane Wakahiu
Sauti za wanwake katika nafasi za umma

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.

07 Agosti 2026, 11:45