Sudan:Paroko wa Parokia auawa baada ya kuripoti wizi wa dawa
Vatican News
Padre Youhanna Al-Amin, wa Parokia ya Mtakatifu Vincent huko Kauda, aliuawa Ijuma, tarehe 19 Juni 2026, pamoja na wengine wawili katika Milima ya Nuba, eneo lililokumbwa na mvutano unaoongezeka wa kikabila na migogoro ya ndani kati ya vikundi vyenye silaha. Habari hizo, ambazo pia ziliripotiwa na Shirika la Kipapa la Kanisa Hitaji (ACI) Africa, zikinukuu vyanzo vya ndani vilivyosema uhalifu huo ulikuwa kitendo cha kulipiza kisasi dhidi ya Padre Youhanna, ambaye alikuwa ameripoti wizi wa dawa ambazo Kanisa hilo lilikuwa likiwahifadhia wakazi wa eneo hilo.
Shambulio la Milima ya Nuba
Jinsi vita nchini Sudan vinavyobadilika kuanzia na kuenea Kordofan, matumizi ya ndege zisizo na rubani na hofu ya kipindupindu. Katika mwaka mpya, mgogoro mkubwa zaidi uko Kauda, uliopo katika jimbo la Kordofan Kusini, kitovu kikuu cha Milima ya Nuba kinachodhibitiwa na Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Sudan-Kaskazini. Katika miezi ya hivi karibuni, ACS inaripoti, hali mbaya ya usalama, pamoja na migogoro ya silaha na kikabila, imewalazimisha baadhi ya viongozi wa kidini kuondoka katika eneo hilo. Hata hivyo, Padre Youhanna alichagua kubaki na jamii aliyoihudumia, na kuwa mmoja wa mapadre wachache ambao bado wanafanya kazi katika eneo hili walioathiriwa sana na vurugu. Jukumu lake lilizidi zaidi ya utunzaji rahisi wa kiroho.
Huzuni ya Jimbo Katoliki la El Obeid
Habari za kifo chake zilihuzunisha sana Jimbo zima la El Obeid, ambayo Padre Youhanna aliitumikia kwa karibu miaka thelathini. Aliwasindikiza vizazi vya waamini, na kuwa mtu mpendwa ndani na nje ya jumuiya ya Wakatoliki. Katika ujumbe wa rambirambi uliopokelewa kutoka Shirika la Kipapa la Kanisa Hitaji kwa, Parokia ya Mtakatifu Petro huko Babnusa (ambapo Padre alihudumu kuanzia 1997 hadi 2021) ilisisitiza kwamba Padre Youhanna alikuwa "rafiki wa vijana na watoto na alipenda kazi yake hadi mwisho." "Leo tunamkumbuka Mchungaji wetu mpendwa Padre Younna, ambaye maisha yake yalichukuliwa kwa huzuni na wale waliochagua vurugu badala ya amani. Padre Younna alijitolea miaka mingi ya huduma ya uaminifu kwa watu, akiwapa matumaini, mwongozo, na huruma wote. Urithi wake wa upendo, na kujitolea kwa wanadamu utaendelea kuwatia moyo vizazi,” inasomeka sala iliyotungwa na jumuiya ya Wakristo wa Milima ya Nuba.
Sudan, sura ya nchi iliyoharibiwa na miaka mitatu ya vita
Kifo cha Padre Youhanna Al-Amin (ambacho Kanisa la eneo hilo limeomba uchunguzi wa kina) kinaongeza mfululizo wa matukio ya vurugu ambayo yameathiri Kanisa nchini Sudan katika miaka ya hivi karibuni. Mnamo Juni 2025, Padre Luka Jomo, Padre wa Jimbo la El Obeid, aliuawa kwa risasi iliyopotea wakati wa shambulio dhidi ya mji wa El Fasher, mji mkuu wa Mkoa wa Darfur Kaskazini. Miezi michache iliyopita, Askofu wa El Obeid, Yunan Tombe Trille Kuku Andali, alikuwa amepigwa kikatili na watu wenye silaha alipokuwa akirudi Jimboni na kupata majeraha makubwa.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here.