Papa Leo XIV,Hospitali ya magonjwa ya akili:Ziara ya Papa itasaidia kujumuisha wote!
Na Joseph Tulloch – Malabo.
Katika Hospitali ya Magonjwa ya Akili ya Jean-Pierre Olie huko Malabo, Guinea ya Ikweta, maandalizi yaliendeliwa vizuri kwa ajili ya kufika kwa Papa Leo XIV. Nembo rasmi ya ziara ya Papa, yenye kauli mbiu: "Kristo, nuru ya Guinea ya Ikweta, kuelekea mustakabali wa matumaini", ilibandikwa nje ya majengo, na safu za viti zimechorwa katika banda la kati ambapo wagonjwa na wafanyakazi wangekusanyika kusikiliza kutoka mawaidha kutoka kwa Papa. "Ni heshima kubwa", alisema Profesa Bechir Ben Hadj Ali, daktari wa Tunisia ambaye anahudumu kama Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali hiyo. Ziara ya Papa ni "ishara muhimu sana", alisisitiza, ambayo alisema inaakisi umuhimu wa afya ya akili nchini Guinea ya Ikweta na duniani kote.
Wagonjwa 125 wanaume kwa wanawake wenye ugonjwa wa akili,mfadhika na uraibu
Kituo hicho, ambacho ni cha aina yake pekee nchini, kilianzishwa muongo mmoja uliopita, mwanzoni kikiwa na vitanda 25 pekee. Kwa sasa kina vitanda 146, vilivyogawanywa katika Wodi sita. Kwa sasa, kinawatunza wagonjwa wapatao 125 (wanaume 100 na wanawake 25) wanaoishi na ugonjwa wa akili, mfadhaiko, wasiwasi, na uraibu wa dawa za kulevya. Mnamo Desemba 2025, Hospitali hiyo ilibadilishwa jina kwa heshima ya Daktari maarufu wa magonjwa ya akili wa Ufaransa Jean-Pierre Olié, ambaye alikuwa mhusika mkuu katika kukianzisha.
Kutelekezwa wenye magonjwa ya akili
Msaada wa Mke wa Rais Constancia Mangue de Obiang pia ulikuwa muhimu, alisema Profesa Ben Hadj Ali. Daktari huyu wa Tunisia alisisitiza, kwamba duniani kote, hasa barani Afrika, afya ya akili mara nyingi huchukuliwa kimakosa kuwa sio jambo la muhimu, na kwa hivyo alitumaini ya kwamba ziara ya Papa itatuma ujumbe ulio mzito kuhusu umuhimu wa kuwatunza wale wanaougua magonjwa ya akili. Daktari Engracia Asangono Nchuchuma, Naibu Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, alielezea kwamba muundo huo hivi karibuni umebadilika kuelekea mfumo wa huduma inayotegemea jamii. Hospitali hiyo haitoi tu ushauri wa magonjwa ya akili na kisaikolojia kwa wagonjwa kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa, bali pia ina timu inayoyoenda nje na kuwatembelea na kuwahudumia wagonjwa ambao, kwa sababu mbalimbali, hawawezi kuhudhuria uchunguzi wao wa kimatibabu.
Ujio wa Papa Leo XIV utasaidia kuwatambua na kuwajali wagonjwa wote bila kuwatenga
Zaidi ya hayo, hivi karibuni imefungua kitengo cha magonjwa ya akili kwa watoto ili kushughulikia mahitaji yanayoongezeka miongoni mwa watoto wadogo. Juhudi zinafanywa pia ili kukidhi mahitaji ya kiroho ya wagonjwa, alisema Dk. Asangono Nchuchuma, ikiwa ni pamoja na sherehe za Misa na maandalizi ya ziara ya Papa. Ujio wa Papa Leo XIV, alisisitiza, "utasaidia kila mtu kuwaona watu wenye magonjwa ya akili si kama watu binafsi wa kutengwa, bali kujumuika katika jamii zetu."
Imesasishwa tarehe 24 Aprili 2026 saa 7:54 mchana na Sr Christina Masivo.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.