Tafuta

Maaskofu wa Antille walikutana na Papa mjini Vatican Aprili 30 Maaskofu wa Antille walikutana na Papa mjini Vatican Aprili 30   (ANSA)

Maaskofu wa Antilles waleta uhalisia wa Caribbean moyoni mwa Kanisa la Ulimwenguni

Rais wa Baraza la Maaskofu wa Antilles alielezea ziara ya kichungaji ya Maaskofu mjini Vatican na Roma kama wakati muhimu wa ushirika na Kanisa la Ulimwengu na fursa ya kushiriki ukweli wa kichungaji wa Caribbean.Alisema hayo wakati wanajiandaa na hija ya Kichungaji mjini Vatican ambapo watakutana na Baba Mtakatifu Leo XIV

Vatican News

Askofu Mkuu Charles Jason Gordon, Rais wa Baraza la Maaskofu wa Antilles (AEC) alielezea ziara ya kichungaji (La visita ad limina Apostolorum,)  mjini Vatican na Roma, kama wakati wa bahati na upendeleo wa ushirika, kukutana, na kubadilishana kati ya Makanisa ya eneo la Caribbean na Kanisa la Ulimwengu. Akizungumza na Vatican News wakati wa ziara ya Maaskofu  hao, Askofu Mkuu Gordon alitafakari umuhimu wa ziara hiyo akiiita, "wakati maalum sana katika maisha ya Askofu, na katika maisha ya Baraza la Maaskofu." Askofu Mkuu, ambaye pia alihudumu kama Askofu Mkuu katika Bandari ya Hispania, alibainisha kuwa ziara hiyo inawapatia Maaskofu fursa ya kipekee ya kukusanyika mji wa Vatican na kushirikishana moja kwa moja na mabaraza ya  Curia Romana.

Wakati wa ushirika na kusikiliza

"Tunakuja Vatican, ili kupata ushirika, kusikiliza kwa undani mapigo ya moyo wa Kanisa lakini pia kushirikisha upekee wa utume katika muktadha wetu na Mabaraza tofauti tunayokutana nayo. Kwa kufafanua kwa ujumla  juu ya asili ya mkutano wa kichungaji, Askofu Mkuu Gordon alisema mabadilishano kati ya Kanisa la Ulimwengu na mahalia yanaimarisha yote mawili. "Kanisa ni la Ulimwengu wote, lakini pia Kanisa mahalia," alisema. "Katika mazungumzo haya kati ya ulimwengu wote na mahalia, daima kuna utajiri mkubwa ambao tunaondoka nao.” Askofu Mkuu huyo alielezea kwamba uzoefu wa Makanisa mahalia pia unaweza kusaidia Kanisa la Ulimwengu wote kutafakari kwa undani zaidi kuhusu hali halisi ya kichungaji kutokana na  mitazamo mipya

Kuinjilisha bara la kidijitali

Miongoni mwa mikutano ya kwanza ya ziara ya Maaskofu wa Caribbean(Karibi)ilikuwa mkutano na Baraza la Mawasiliano, ambapo majadiliano yalizingatia utume wa Kanisa katika ulimwengu wa kidijitali. Askofu Mkuu Gordon alisisitiza kwamba ingawa mitandao ya kijamii inaleta hatari zisizopingika, hatari hizo haziwezi kuzuia Kanisa kuinjilisha katika nyanja ya kidijitali. "Kuna hatari katika mitandao ya kijamii," alisema, "lakini kuna hatari zinazovuka barabara, hatari zinazosafiri kutoka sehemu moja ya nchi hadi nyingine. Hatari hizo haziwezi kutuzuia kupeleka Injili kwa wote, katika nyanja zote za maisha na shughuli."

Akirudia maelezo ya Papa Benedikto XVI kuhusu intaneti/mtandao wa watu  kama "bara la kidijitali," Askofu Mkuu Gordon alisema Kanisa lazima likubali jukumu lake la kimisionari mtandaoni. "Ni mahali ambapo tunapaswa kuwa wamisionari pia, sio tu kupeleka ujumbe huko, bali pia kuunda mwingiliano katika vyombo vya habari vya kidijitali." Alielezea kwamba Wakristo wameitwa kusaidia kuhakikisha mawasiliano ya kidijitali yanakuwa "ya kibinadamu zaidi" na "yanayofanya watu kuwa waadilifu zaidi," ili nafasi za mtandaoni ziweze kuwaongoza watu vyema katika utafutaji wao wa ukweli na maana.

Akielezea changamoto za Karibi Roma

Akigeukia hali halisi inayokabili Kanisa huko Karibi, Askofu Mkuu Gordon aliakisi udhaifu wa tabianchi,  uhamiaji, na maisha ya familia kama miongoni mwa mambo muhimu zaidi ya kichungaji katika eneo hilo. "Katika eneo letu, sisi ndio eneo la pili lililo hatarini zaidi kwa mabadiliko ya tabianchi, na hilo huwa suala kubwa kila wakati," alisema, akibainisha vitisho vikubwa vinavyotokana na kuongezeka kwa viwango vya bahari, vimbunga, na uharibifu wa mazingira kwa mataifa ya Karibi(Carribbien). Uhamiaji pia, unabaki kuwa changamoto kubwa. Akikumbuka athari za mgogoro wa Venezuela na ukosefu wa utulivu wa kikanda, Askofu Mkuu Gordon alisema nchi kama vile Trinidad na Tobago zimepokea "maelfu na maelfu ya wahamiaji" kutoka Venezuela, Haiti, Cuba, na kwingineko katika Karibian na Amerika Kusini. Pia alizungumzia uzoefu wa kipekee wa kihistoria wa maisha ya familia ya Karibian, ulioundwa na karne za ukoloni na mfumo wa upandaji miti. "Tumekuwa na muundo wa miaka 400 wa familia zilizovurugwa kupitia mfumo wa upandaji miti," alielezea, akibainisha kuwa hii imezalisha mienendo ya familia na hali halisi ya uchungaji tofauti na sehemu zingine nyingi za dunia.

Changamoto kama fursa za neema

Askofu Mkuu Gordon alisema kusudi la kuleta hali halisi hizi Vatican si tu kuleta matatizo, bali kuchangia uzoefu maalum wa Karibi katika utambuzi mpana wa Kanisa. "Matumaini ni kuleta upekee huu, upekee huu, kwenye mazungumzo ya ulimwengu wote," alisema. Kwa kufanya hivyo, aliongeza, maaskofu wanatafuta kupokea na kutoa mwanga ambao unaweza kusaidia kubadilisha changamoto kuwa fursa za utume. "Kuona utume wetu na kuona changamoto," alisema, "sio kama changamoto tu, bali pia kama neema na fursa za uinjilishaji."

Imesasishwa tarehe 30 Aprili 2026 saa 8.15 mchana na Angella Rwezaula.

MAASKOFU WA ANTILLES

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.

29 Aprili 2026, 11:20