Kard.Pizzaballa:Yerusalemu yaitwa kuponya majeraha ya dunia
Na Sr. Christine Masivo, CPS – Vatican.
Wakristo wanapaswa kuishi vipi katikati ya mgogoro unaoikumba Nchi Takatifu kwa sasa? Hilo ndilo swali lililo katikati ya barua mpya ya kichungaji kutoka kwa Patriaki wa Kilatini wa Yerusalemu, Kardinali Pierbattista Pizzaballa. Ni ujumbe uliochapishwa Jumatatu tarehe 27 Aprili, 2026, barua hiyo yenye kichwa: "Walirudi Yerusalemu kwa furaha kubwa: Pendekezo la kuishi wito wa Kanisa katika Nchi Takatifu."
Kuponya majeraha ya dunia
Wito wa Yerusalemu, Kardinali Pizzaballa alibainisha katika maandishi, ni kuponya majeraha ya dunia. Tafakari ya Patriaki ilizunguka taswira ya mji wa Yerusalemu wa Biblia, ambao "uliashiria kuishi pamoja na uhusiano, wa kiraia na wa kidini." Barua hiyo ilipangwa katika sehemu tatu: ya kwanza ikiwa ni tathmini ya hali ya sasa ya eneo hilo, ya pili ni maono kwa Kanisa la Yerusalemu, na ya tatu inaakisi athari za kichungaji kwa parokia, familia, shule, na taasisi. Kardinali Pizzaballa alisisitiza kwamba barua hiyo haina uchambuzi wa kisiasa pekee: ni "kisiasa" kwa maana pana zaidi, kwa kadiri inavyohusu kubaki kwetu, kama Wakristo, ndani kiungo cha kisiasa au ulimwengu uliopo, huku ikilenga kila sera za kiasia za kweli na za uhakika, Yerusalemu ya mbinguni.
Matukio ya maji
Patriaki Pizzaballa aliaseme mgogoro ulioanza kutokea 7 Oktoba 2023 na vita huko Gaza "matukio ya maji yaliyofunga enzi moja na kufungua nyingine, yakifanya hivyo kwa njia mbaya zaidi. Tunachopitia si mgogoro wa ndani tu, alisema. "Mgogoro wa ndani ni dalili ya mgogoro mkubwa zaidi, mabadiliko ya dhana ya kimataifa. Kwa miongo kadhaa, jumuiya ya kimataifa, na hasa ulimwengu wa Magharibi, uliamini katika utaratibu wa kimataifa unaotegemea sheria, mikataba, na ushirikiano wa pande nyingi ... Leo, kila mtu anaonekana kuamka na udhaifu katika mfumo huu." "Tunashuhudia utegemezi mpya wa matumizi ya nguvu kama njia muhimu ya kutatua migogoro," Pizzaballa aliandika. "Vita vimekuwa kitu cha ibada ya sanamu"
Matokeo ya machafuko
Katika vita pia vinavyoendeshwa kwa maneno na picha, Patriaki alibainisha, inazidi kuwa vigumu kutofautisha "habari na propaganda". Patriaki wa Yerusalemu alipitia matokeo ya machafuko haya, aliandika, katika kuvunjika kwa mahusiano yaliyochochewa na chuki na kutoaminiana, na kugawanyika katika maeneo na viputo vya utambulisho vinavyoongezwa na algoriti za mitandao ya kijamii. Miongoni mwa athari mbaya pia ni mgogoro wa mazungumzo kati ya dini: "Mahali Patakatifu, ambayo yanapaswa kuwa mahali pa maombi, yanakuwa viwanja vya mapigano kuhusu utambulisho. Maandiko matakatifu yanaombwa kuhalalisha vurugu, uvamizi, na ugaidi." "Ninaamini matumizi mabaya haya ya jina la Mungu ndiyo dhambi kubwa zaidi ya wakati wetu," Pizzaballa aliandika.
Taswira ya Vatican
Kujibu hali hiyo, Patriaki Pizzaballa alisema, Kanisa la Yerusalemu "limeifanya sauti yake isikike, likijaribu kusema neno la ukweli – lililo la kweli, wazi, kwa ujasiri - hata katikati ya machafuko haya, mara nyingi kwa gharama ya kutoelewana." Lakini, aliongeza na kusema kwamba, alijiuliza ikiwa hii imetosha - au kama, "katika kipindi hiki chenye changamoto nyingi, je, wakati mwingine tumechagua busara na kutafuta kuishi kitaasisi, tukitoa kafara ushuhuda wetu wa kinabii? ... Ni swali linalonisumbua kila siku, na ambalo si rahisi kujibu."
Kardinali Pizzaballa aliandika kwamba mtu lazima pia ajiulize kwamba, ni nini mapenzi ya Mungu kwa Yerusalemu? Yerusalemu "sio suala la mipaka ya kisiasa au mipango ya kiufundi tu", lakini "utambulisho wake mkuu - sifa muhimu zaidi ya jiji na Nchi Takatifu nzima - ni ile ya kuwa mahali pa ufunuo wa Mungu, mahali ambapo imani ziko nyumbani." Kwa kupuuza mwelekeo huu ulio na msimamo kidete wa Nchi Takatifu, "unyeti wa kidini na kiroho wa jamii zinazoishi ndani yake" ndio "sababu kubwa zaidi ya kushindwa kwa makubaliano ya kuishi pamoja ambayo yamefanyika katika miongo ya hivi karibuni," alisisitiza Patriaki.
Athari za kichungaji
Katika ngazi ya kichungaji, Kardinali Pizzaballa alisisitiza umuhimu wa liturujia na sala. Kimsingi ni jukumu la familia kama vile warsha za elimu katika kuishi pamoja na heshima, ambapo yaliyopita yanaweza kupitishwa kwa watoto kwa huzuni na ukweli, bila kuchochea hisia za chuki na kisasi. Shule za Kikristo zinapaswa kueleweka kama "warsha za ubinadamu mpya", ambapo watoto huelimishwa kusoma historia tena kwa macho yasiyo na chuki, Kardinali Pizzaballa aliandika. Hospitali na huduma za kijamii ni mahali ambapo kukaribishwa, mazungumzo, na uponyaji tayari yanakuwa ukweli ulio hai na ni lazima ziungwe mkono. Patriaki alisema kwamba jukumu muhimu pia ni la wazee, ambao ni kumbukumbu hai; kwa vijana, ambao ni unabii; na kwa mapadre na watawa, ambao ni marejeleo wa uaminifu kwa jamii na mifano ya uwezekano wa kuishi pamoja. Hatimaye, Kardinali Pizzaballa alisema, mazungumzo kati ya dini pia yanabaki kuwa "hitaji muhimu."
Kama wanafunzi baada ya kupaa
Akihitimisha barua hiyo, Patriaki Pizzaballa aliandika kwamba ni muhimu kukataa "ushiriki wowote na utamaduni wa vurugu," huku akitoa nafasi ya kuaminiana. Yote haya yanawezekanaje? Jibu ni rahisi: labda, si hivyo peke yake. Lakini hatuko peke yetu." Yesu anatusubiri, Patriaki alisema, katika Parokia zetu, katika jumuiya zetu za imani, katika vikundi vyetu na harakati za Kikanisa. "Mwishowe, kinachotutegemeza si nguvu zetu wenyewe, bali furaha ya Injili," alisisitiza. "Turudi Yerusalemu kwa furaha. Turudi maishani mwetu kwa shauku. Tubebe mioyoni mwetu ndoto ya Mungu kwa Mji wa Mungu, na turuhusu ndoto hiyo iwe, hatua kwa hatua, siku baada ya sikuna iwe maisha yetu,"alihitimisha Kardinali Pizzaballa.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.