Tafuta

2026.04.28 Siku ya IX ya Vijana Kimajimbo nchini Guinea-Bissau. 2026.04.28 Siku ya IX ya Vijana Kimajimbo nchini Guinea-Bissau. 

Guinea-Bissau:Maelfu ya vijana washerehekea Siku ya IX ya Vijana Wakatoliki kimajimbo!

Zaidi ya vijana elfu tano na baadhi ya waamini Wakatoliki wa Guinea-Bissau kutoka majimbo mawili, Jimbo la Bafatá na Jimbo la Bissau ya nchi hiyo,walishiriki katika Siku ya 9 ya Vijana Wakatoliki kimajimbo.Tukio hilo la siku tatu,mwishoni mwa Juma kuanzia Aprili 24-26,liliambatana na kumbukumbu ya miaka 25 ya kuanzishwa kwa Jimbo la Bafatá.

Na Casimiro Jorge Cajucam – Bissau.

Kwa kuongozwa na  kauli mbiu "Imani, Upendo na Matumaini,"jiji la Bafatá lilipitia siku tatu zilizojaa hali ya kiroho, furaha, na ushirika. Licha ya joto kali, ambalo lilikuwa kati ya nyuzi joto 42 na 43 kipimo cha Selsiasi, shauku na uchangamfu wa washiriki haikupungua. Shughuli zilianza Ijumaa alasiri, tarehe 24 Aprili ambapo vijana walikaribishwa na kusalimiwa na Askofu Vítor Quematcha wa Bafatá, na kufuatiwa na usiku ya kuabudu mbele ya Ekaristi Takatifu. Askofu Quematcha alitoa Katekesi yake kwa vijana na familia za waamini Wakatoliki waliohudhuria. Baadaye, Askofu José Lampra Cá wa Bissau aliadhimisha Ibada ya Misa Takatifu.

Misa wakati wa kuhitimisha Sikku ya Vijana wa Guinea Bissau
Misa wakati wa kuhitimisha Sikku ya Vijana wa Guinea Bissau

Maaskofu na Mwakilishi wa Vatican walitembelea gereza

Kabla ya kuadhimisha Misa Takatifu, wafungwa katika Kituo cha Gereza la Bafatá walitembelewa na viongozi kadhaa wa Kanisa, akiwemo Askofu José Lampra Cá, Askofu José Câmnate na Bissiga (Askofu Mstaafu wa Bissau), na Balozi wa Vatican nchini  Guinea Bissau Askofu Mkuu Waldemar Stanislaw Sommertag, akiambatana na mapadre kadhaa. Wakati wa ziara hiyo, wafungwa walipokea zawadi ya  mashati yenye mada ya Jubilei  na vitu vya Siku ya Vijana, pamoja na vifaa vya usafi wa binafsi. Mpango huu ulikusudiwa kuonesha ukaribu na mshikamano wa Kanisa, na wafungwa.

Vijana wa Bissau
Vijana wa Bissau

Misa ya kufunga, iliyofanyika siku ya Dominika, tarehe 26 Aprili 2026 iliongozwa na Balozi wa Vatican nchini Guinea Bissau,  Askofu Mkuu Sommertag, huku mahubiri yakitolewa na Askofu Vítor Luís Quematcha. Katika ujumbe wake, Askofu alisisitiza kwamba "kumfuata Kristo si hisia ya kidini tu bali ni uamuzi wa maisha." Aliongeza kuwa, "katika muktadha wa Guinea, hii ina maana ya kuchagua ukweli badala ya uongo, na haki badala ya ufisadi."

Nchi inahitaji vijana wake

Askofu Vítor Quematcha aliwakumbusha vijana kwamba "Kanisa linawaamini na kwamba nchi inahitaji kujitolea kwao," aliwomba wawe na ujasiri na matumaini. Pia aliwasalimia familia zilizokuwepo, na alisisitiza kwamba "jukumu lao la msingi kama nafasi ya kusambaza imani, upendo, na uwajibikaji." Askofu huyo pia alikabidhi Jimbo la Bafatá na Bissau zikijiandaa kusherehekea jubilei ya miaka 50 mwaka ujao kwa Mchungaji Mwema. Katika kuaga na baraka ya mwisho, Askofu Mstaafu wa Bissau, José Câmnate na Bissign, aliwasihi watoto wanaokwenda shuleni na vijana kuchukua jukumu kubwa katika kuhamaisha upatanisho na amani nchini Guinea-Bissau.

Balozi wa Vatican Nchini Guinea Bissau aliudhuria
Balozi wa Vatican Nchini Guinea Bissau aliudhuria

Imesasishwa na tarehe 30 Aprili 2026 saa 5.50. na Christine Masivo, CPS – Vatican.

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.

30 Aprili 2026, 11:48