Tafuta

2026.03.17 Rwanda - Mkutano wa Maaskofu wa Rwanda naBurundi umehitimishwa kwa Mada ya "Kukamilisha Mkataba wa Elimu barani Afrika. 2026.03.17 Rwanda - Mkutano wa Maaskofu wa Rwanda naBurundi umehitimishwa kwa Mada ya "Kukamilisha Mkataba wa Elimu barani Afrika.  

Rwanda-Burundi:Kufanyia Kazi Utekelezaji wa Mkataba wa Elimu wa Afrika

Maaskofu wa Rwanda na Burundi, waliokusanyika chini ya mwavuli wa Baraza la Maaskofu wa Rwanda na Burundi (ACOREB), wakiazimia kutekeleza Mikataba ya Elimu ya Dunia na Afrika katika shule za Kikatoliki za nchi zote mbili. Walifikia uamuzi huu mwishoni mwa mkutano wao wa hivi karibuni mjini Kigali,Rwanda.

Profesa Jean-Paul Niyigena – Kigali na Sr. Christine Masivo, CPS - Vatican

Makanisa ya Burundi na Rwanda yana mtandao mpana wa shule za Kikatoliki zinazohudumia ngazi zote za elimu. Hizi ni pamoja na shule za awali, shule za msingi, shule za upili, shule za ufundi, na taasisi nyingi za juu kama vile vyuo vikuu. Kwa azimio hili, maaskofu wanaitikia wito wa Papa Leo XIV wa kutathmini dhamira ya shule za Kikatoliki barani Afrika, kwa kuzingatia changamoto nyingi za bara hilo. Viongozi wengi wa kisiasa wa Afrika wamehudhuria shule za Kikatoliki, na kufanya wito huu wa kuchukua hatua kwa wakati unaofaa zaidi.

Mkutano wa Maaskofu wa Rwanda na Burundi kuhusu Mkataba wa Elimu Afrika
Mkutano wa Maaskofu wa Rwanda na Burundi kuhusu Mkataba wa Elimu Afrika

Elimu ya Kikatoliki kwa mabadiliko ya Kijamii

Maaskofu wanataka elimu ya Kikatoliki katika nchi zao itegemee kufundisha maadili ya kibinadamu na ya Kikristo ambayo, walieleza kuwa kwa sasa yamekuwa madhaifu hasa katika eneo la Maziwa Makuu. “ Kwa kuwa Mkataba wa Elimu wa Afrika ni mwongozo, Kanisa lazima liendeleze elimu kamili, inayodumisha maarifa, tabia, na huduma," Maaskofu walithibitisha. Kisha wakajitolea kuboresha ubora wa elimu kwa kuwafundisha vijana kumthamini kila mtu na kuwajali walio katika mazingira magumu.

Maaskofu wa Rwanda na Burundi wakati wa Misa
Maaskofu wa Rwanda na Burundi wakati wa Misa

Kwa lengo hili, maaskofu wa nchi zote mbili wanataka kufanya tathmini ya kina ya mifumo yao ya elimu haraka iwezekanavyo, kwa matumaini ya "kuifanya elimu ya Kikatoliki kuwa kichocheo halisi cha mabadiliko ya kijamii" katika nchi zao husika. Mchakato huu utachukua umbo la Mikutano Mikuu ya Elimu ya Kikatoliki, ambayo Makanisa hayo mawili kwa undugu yanapanga kuandaa katika siku za usoni.

Wakati wa Misa baada ya Mkutano wao maaskofu wa Rwanda na Burundi
Wakati wa Misa baada ya Mkutano wao maaskofu wa Rwanda na Burundi

Mpango mpana Uliwenguni kote

Zaidi ya hayo, Maaskofu wanakusudia kuhamasisha jumuiya nzima ya elimu ya Kikatoliki kuzunguka Mkataba wa Elimu wa Kimataifa na Mkataba wa Elimu wa Afrika. Wameweka malengo mawili ya muda mfupi: kuhakikisha usambazaji wa mkutano huu wa kikanisa na kuanzisha tume ya kutengeneza miongozo muhimu kwa ajili ya utekelezaji wake. Mkutano wa pamoja wa Maaskofu wa Rwanda na Burundi, uliongozwa na Kardinali Antoine Kambanda, Askofu Mkuu wa Kigali, na Askofu Joachim Ntahondereye, wa jimbo la Muyinga nchini Burundi. Kutekeleza Mkataba wa Elimu Duniani na Mkataba wa Elimu wa Afrika kunafuatia juhudi ambazo tayari zimefanywa na mikutano mingine ya Maaskofu wa Afrika, ikiwa ni pamoja na ile ya Nigeria na Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Kardinali Antoine Kambanda, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Kigali Rwanda
Kardinali Antoine Kambanda, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Kigali Rwanda
RWANDA NA BURUNDI ELIMU

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku bonyeza hapa: Just click here.

 

23 Machi 2026, 09:42