Rwanda-Burundi:Kufanyia Kazi Utekelezaji wa Mkataba wa Elimu wa Afrika
Profesa Jean-Paul Niyigena – Kigali na Sr. Christine Masivo, CPS - Vatican
Makanisa ya Burundi na Rwanda yana mtandao mpana wa shule za Kikatoliki zinazohudumia ngazi zote za elimu. Hizi ni pamoja na shule za awali, shule za msingi, shule za upili, shule za ufundi, na taasisi nyingi za juu kama vile vyuo vikuu. Kwa azimio hili, maaskofu wanaitikia wito wa Papa Leo XIV wa kutathmini dhamira ya shule za Kikatoliki barani Afrika, kwa kuzingatia changamoto nyingi za bara hilo. Viongozi wengi wa kisiasa wa Afrika wamehudhuria shule za Kikatoliki, na kufanya wito huu wa kuchukua hatua kwa wakati unaofaa zaidi.
Elimu ya Kikatoliki kwa mabadiliko ya Kijamii
Maaskofu wanataka elimu ya Kikatoliki katika nchi zao itegemee kufundisha maadili ya kibinadamu na ya Kikristo ambayo, walieleza kuwa kwa sasa yamekuwa madhaifu hasa katika eneo la Maziwa Makuu. “ Kwa kuwa Mkataba wa Elimu wa Afrika ni mwongozo, Kanisa lazima liendeleze elimu kamili, inayodumisha maarifa, tabia, na huduma," Maaskofu walithibitisha. Kisha wakajitolea kuboresha ubora wa elimu kwa kuwafundisha vijana kumthamini kila mtu na kuwajali walio katika mazingira magumu.
Kwa lengo hili, maaskofu wa nchi zote mbili wanataka kufanya tathmini ya kina ya mifumo yao ya elimu haraka iwezekanavyo, kwa matumaini ya "kuifanya elimu ya Kikatoliki kuwa kichocheo halisi cha mabadiliko ya kijamii" katika nchi zao husika. Mchakato huu utachukua umbo la Mikutano Mikuu ya Elimu ya Kikatoliki, ambayo Makanisa hayo mawili kwa undugu yanapanga kuandaa katika siku za usoni.
Mpango mpana Uliwenguni kote
Zaidi ya hayo, Maaskofu wanakusudia kuhamasisha jumuiya nzima ya elimu ya Kikatoliki kuzunguka Mkataba wa Elimu wa Kimataifa na Mkataba wa Elimu wa Afrika. Wameweka malengo mawili ya muda mfupi: kuhakikisha usambazaji wa mkutano huu wa kikanisa na kuanzisha tume ya kutengeneza miongozo muhimu kwa ajili ya utekelezaji wake. Mkutano wa pamoja wa Maaskofu wa Rwanda na Burundi, uliongozwa na Kardinali Antoine Kambanda, Askofu Mkuu wa Kigali, na Askofu Joachim Ntahondereye, wa jimbo la Muyinga nchini Burundi. Kutekeleza Mkataba wa Elimu Duniani na Mkataba wa Elimu wa Afrika kunafuatia juhudi ambazo tayari zimefanywa na mikutano mingine ya Maaskofu wa Afrika, ikiwa ni pamoja na ile ya Nigeria na Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku bonyeza hapa: Just click here.