Tafuta

2026.02.09 Uwakilishi wa Baraza la Kipapa la Huduma ya Maendeleo Fungamani ya ya Binadamu huko Chiclayo. 2026.02.09 Uwakilishi wa Baraza la Kipapa la Huduma ya Maendeleo Fungamani ya ya Binadamu huko Chiclayo. 

Peru:Siku ya Wagonjwa huko Chiclayo,pamoja na mwili ni kutunza na roho

Kuanzia tarehe 9 hadi 11 Februari 2026 katika Toleo la XXXIV la tukio la Kimataifa,kwa uwepo wa Kardinali Michael Czerny,Mwakilishi wa Papa Leo XIV, yuko katika Jimbo alilokuwa kama Askofu kuadhimisha Siku ya Wagonjwa Duniani."Tusipohakikisha huduma inayojumuisha upande wa kiroho,tutajikuta hatujakamilika na kuwa na athari kubwa kwa afya ya kaka na dada zetu."Ni kauli ya Dk. Walder Carpio,mratibu wa Huduma ya Kichungaji ya Afya katika Jimbo la Chiclayo,Kaskazini mwa Peru.

Sebastian Sanson Ferrari na Angella Rwezaula–Vatican.

"Tusipohakikisha huduma inayojumuisha upande wa kiroho, tutajikuta hatujakamilika na kuwa na athari kubwa kwa afya ya kaka na dada zetu." Hii ni kauli ya Dk. Walder Carpio, mratibu wa Huduma ya Kichungaji ya Afya katika Jimbo la Chiclayo, Kaskazini mwa Peru, ambayo inaandaa Siku ya XXXIV ya Wagonjwa Duniani, kuanzia tarehe 9 hadi 11 Februari 2026. Hii ni Chiclayo ambapo Askofu Robert Francis Prevost, leo hii ni Papa Leo XIV alifanya huduma yake ya Kichungaji kama mmisionari na Askofu. Anayemwakilisha Papa katika tukio la Kimataifa nchini Peru ni Kardinali Michael Czerny, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Kuhamasisha Maendeleo Fungamani ya Binadamu, aliyeteuliwa kuwa mjumbe maalum wa Baba Mtakatifu. Kardinali alifika Chiclayo siku chache zilizopita akiwa na ujumbe kutoka Baraza la Kipapa na ratiba yake ya kukutana na wawakilishi wa Kanisa mahalia, ambao wataweza kuwasilisha kazi yao kwa niaba ya wagonjwa na waliotengwa, kwa kuzingatia huruma hai na utunzaji kamili.

Ukaribu unaokuwa hatua ya matendo mema

Carpio ni mmoja wa hawa. Wakati wa janga la Uviko-19, alipokuwa akiongoza Hospitali ya Almanzor Aguinaga Asenjo, alikutana na Askofu Prevost wa wakati huo, ambaye alifika kwa ziara ya ghafla. "Alitembea kwenye Korido akiwa na hatua zote muhimu za usalama, akawabariki wafanyakazi, na kutoa takriban rozari 500 kwa wafanyakazi na wagonjwa," daktari alikumbuka hayo akizungumza na Vyombo vya habari vya Vatican. "Hakutujaza matumaini tu, bali pia alitufundisha kwamba ukaribu wa kweli na mateso unahitaji uwepo na unyenyekevu. Rozari hizo zilituliza maumivu na kuimarisha kujitolea kwetu, zikituunganisha na upendo wa Kristo na Mama Yetu." Kwa Jimbo la kaskazini mwa Peru, urithi wa Askofu Prevost unabaki kuwa mwongozo: "Alitufundisha kwamba huduma ya kichungaji kwa wagonjwa haiwezi kupunguzwa kwa huduma ya matibabu, lakini lazima ijumuishe vipimo vya kisaikolojia, kijamii, na kiroho. Ni kwa njia hiyo tu huduma inaweza kuwa pana kweli."

L'accoglienza a Chiclcayo per il cardinale Czerny

Kupokelewa kwa Kardinali Czerny huko Chiclcayo

Hali ya Afya nchini Peru

Dk. Carpio pia alieleza ugumu wa mfumo wa huduma ya afya wa Peru: "Ni mfumo uliogawanyika... Wizara ya Afya, kupitia Bima ya Afya ya Nyongeza, inashughulikia takriban 70% ya idadi ya watu. Pia kuna sekta ndogo za kibinafsi, lakini upatikanaji wa huduma bora bado ni changamoto. Watu wengu wa Peru wana aina fulani ya bima, lakini kwa vitendo, watu wengi hupuuzwa haki zao na hubaki nyumbani bila kupata huduma wanayohitaji." Kwa hivyo, kazi ya Wizara ya Afya ya Kichungaji inajumuisha mwelekeo, usaidizi, na elimu ya afya, kuhakikisha kwamba huduma inawafikia wale wanaouhitaji zaidi. Kwa daktari, huduma kamili haizuiliwi tu kuponya mwili: "Lazima izingatie kipimo cha kibiolojia, kipimo cha kisaikolojia, usaidizi wa kifamilia na kijamii, na, zaidi ya yote, kipimo cha kiroho. Hata wagonjwa wasio Wakatoliki hupata faraja wanapopewa nafasi ya kutafakari na matumaini. Huu ndio mabadiliko halisi katika kupona kwao."

Msukumo kwa Siku ya Wagonjwa duniania

Siku ya Wagonjwa Duniani inalenga kutoa fundisho hili: kusindikiza wale wanaoteseka kwa muda, kusikiliza, ukaribu, na kujitolea kiroho, na kuhakikisha kwamba huduma ya afya inaunganisha nyanja zote za mwanadamu. " kwa mfano wa  Papa Prevost  wa wakati ule alisema "ulitufundisha kwamba imani hubadilika kuwa uwepo," alielezea mtaalamu huyo. "Tunapogusa upande wa kiroho, huduma ya afya huacha kuwa ya kiufundi tu na inakuwa huduma ya kibinadamu na huruma."

Uwakilishi wa Baraza la Kipapa la Maendeleo Fungamani ya Binadamu huko Chiclayo
Uwakilishi wa Baraza la Kipapa la Maendeleo Fungamani ya Binadamu huko Chiclayo

Afya kama kukutana

Huko  Jimboni Chiclayo, Parokia na hospitali hufanya kazi, kwa kifupi, kufuata mafundisho yaleyale: kuwa karibu na wale wanaoteseka ni kitendo halisi, kinachohitaji hatua na moyo wazi. Mbali na usaidizi wa kichungaji, Siku ya Wagonjwa Duniani inaalika tafakari kuhusu mifumo ya huduma ya afya. Mihadhara na vikao vya kitaaluma vitashughulikia mada kama vile huduma ya kupunguza maumivu na usimamizi wa mateso katika utendaji wa kitaaluma, kwa lengo la kuwatia moyo mamlaka na wataalamu kuunganisha huduma kamili kama kiwango.

Kardinali Czerny akiwasalimia wagonjwa
Kardinali Czerny akiwasalimia wagonjwa
Uwakilishi wa Baraza la Kipapa la Maendeleo Frunagamani ya Binadamu huko Chiclayo
Uwakilishi wa Baraza la Kipapa la Maendeleo Frunagamani ya Binadamu huko Chiclayo

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku: Just click here.

10 Februari 2026, 11:47