Ni zana gani zinahitajika kwa amani isiyo na silaha na inayoondoa silaha?
Vatican News
"Amani iwe nanyi nyote: kuelekea amani isiyo na silaha na kupokonya silaha:"huu ndiyo upeo uliooneshwa na Papa Leo XIV katika Ujumbe wake wa Siku ya 59 ya Amani Duniani. Lakini hili linawezaje kupatikana, katika wakati ulioakisiwa na kurudi kwa vita kama chombo cha pamoja cha utatuzi wa migogoro, kudhoofika kwa taasisi za pande nyingi, na msukumo unaoongezeka wa silaha? Swali hili lilikuwa lengo la mkutano wa l, uliotangazwa na Taasisi ya Sheria ya Amani ya Kimataifa ya Giuseppe Toniolo, Chama cha Vijana cha matendo ya Kikatoliku, Italia, Chuo Kikuu cha Kipapa cha Lateran, na Jukwaa la Kimataifa la Matendo ya Kikatoliki. Mkutano huyo ulijikita kuchunguza athari za kisiasa, kiutamaduni, na kijamii za amani ambayo inazidi kutokuwepo kwa vita, lakini inakubali upokonyaji silaha kama kigezo cha hatua za umma na mahusiano ya kimataifa. Haya ni matarajio imara na ya ujasiri, kwa kuzingatia enzi ya kisasa iliyoainishwa na angalau migogoro 56 inayoendelea duniani kote, kama ilivyoainishwa katika utangulizi wa Giuseppe Notarstefano, rais wa kitaifa wa ACI, na Sandro Calvani, rais wa Baraza la Sayansi la Taasisi ya Sheria ya Amani ya Kimataifa ya Giuseppe Toniolo. Akimnukuu Giorgio La Pira, Notarstefano alisema kwamba "tunajikuta katika hatua ya mabadiliko katika historia, ambayo bila shaka inatupa hisia ya kizunguzungu: hatujui tunakoelekea." Hata hivyo, alihitimisha, "Sitaki kurudi nyuma. Hakika, tunataka kupitia kipindi hiki cha kusisimua kwa kufanya kile ambacho vyama vya Kikatoliki hufanya vyema: kuwasaidia watu kutojitenga.
Amani isiyo na silaha: mtindo na ushirika
Kutokana na uhakika huo, kikao cha kwanza cha mkutano kwa mada ya "Amani Isiyo na Silaha: Mtindo na Shirika," kilichukua sura hiyo. Kisha kilishughulikia mizizi ya kiutamaduni na kisheria ya amani. Deborah Tonelli, anayewakilisha Chuo Kikuu cha Georgetown jijini Roma, alitoa tafakari kuhusu kutotumia vurugu kama mtindo wa kibinafsi na kisiasa. Kwa sababu, alisisitiza, "lazima tuache kutazama matukio kwa mantiki ya kibinadamu pekee: Mungu hukaa katika historia yetu. Na, kulingana na hili, hufuatilia njia mpya, hutusaidia kutambua, hufungua upeo mpya na, kwa hivyo, uaminifu. Hili ni muhimu kwa sababu uaminifu huturuhusu kubuni njia mbadala." Kwa hivyo, dhana ya kutotumia vurugu inaibuka, ambayo, kulingana na Tonelli, "inapaswa kueleweka kama nomino mpya: inamaanisha kufungua kitu chanya, katika roho ya watu kama Gandhi, Aldo Capitini, na Mama Teresa wa Calcutta. Zaidi ya hayo, kutotumia vurugu kunamaanisha kuanzisha simulizi ya kawaida ya historia. Kila mmoja wetu anaweza kuchangia kuunda mtindo tofauti wa maisha, ambao hautaondoa uovu, bila shaka, lakini utatusaidia kuweka alama katika kitabu cha historia katika roho ya uaminifu na matumaini."
Ukosoaji mkali wa sababu za vita
Tommaso Greco, profesa wa Falsafa ya Sheria katika Chuo Kikuu cha Pisa, alitoa ukosoaji mkali wa "sababu za vita" ambazo bado zinaenea katika mazungumzo ya umma: "Ukosoaji huu unaanza na ujumbe wa Papa Leo XIV, ambao ni mkali kweli, na unategemea mambo matatu. Kwanza, kuna kukataa kukanusha: kushambulia simulizi kuhusu kutoepukika kwa vita." Kisha, aliendelea, "lazima tutii mwaliko wa Papa wa kujua jinsi ya kutojenga bali kukuza amani. Kwa maana hii, hatimaye, lazima tujue jinsi ya kuthamini zana, kuanzia na sheria za kimataifa pamoja na tabia ya watu binafsi wanaotambua sheria." Aliungwa mkono na Gabriele Della Morte, Profesa wa Sheria za Kimataifa katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Moyo Mtakatifu, ambaye katika hotuba yake alilenga "jukumu la ushirikiano wa pande nyingi, mazungumzo, na uhakika wa sheria za kimataifa kama msingi wa utaratibu wa amani, akianza na mifano ya kila siku ambayo kiukweli inatoka katika mikataba ya kimataifa: pete tano za Olimpiki, nafasi ya mtandao, mwelekeo wa kibinadamu, lakini hata maeneo ya wakati na lugha inayotumika katika ndege."