Greenland:UE wako tayari kujibu tishio la kiuchumi la Trump
Na Roberta Barbi – Vatican.
Wanaiita "ACI," chombo cha kupinga kulazimishwa: kipimo cha kiuchumi cha kukabiliana na ushuru ili kukabiliana na ushuru wa 10% wa Marekani na kusawazisha bajeti ya Ulaya ya bilioni €93. Umoja wa Ulaya(UE) unatumia silaha zake bora dhidi ya tishio la Marekani la kutoza ushuru wa 10% kwa nchi zinazoilinda Greenland, lakini bado haujazitumia: Hatua hizo zimesimamishwa hadi Februari 6, japokuwa uamuzi utafanywa mwanzoni mwa mwezi, ikiwa ni pamoja na ule unaotoa ufikiaji mdogo wa soko la Ulaya kwa makampuni ya Marekani.
Mkutano Maalum wa Baraza la Umoja wa Ulaya(UE)
Mkutano Maalum wa Baraza la Umoja wa Ulaya umeitishwa Alhamisi tarehe 22 Januari 2026 kuhusu suala la Greenland, ili kuthibitisha tena "ahadi yao thabiti kwa kanuni za sheria za kimataifa, uadilifu wa eneo, na uhuru wa kitaifa," alielezea Rais António Costa. Katika taarifa yake, ilirudia "msaada na mshikamano wake wa pamoja na Denmark na Greenland na kutambua maslahi ya pamoja ya nchi za Atlantiki katika amani na usalama katika Aktiki, hasa kupitia NATO." Rais wa Tume ya Ulaya Bi Ursula von der Leyen pia alitoa maoni kuhusu suala hilo kwenye mitandao ya kijamii: "Tutalinda maslahi yetu ya kiuchumi na usalama kila wakati," aliandika. "Tutashughulikia changamoto hizi kwa mshikamano wetu wa Ulaya kwa uthabiti na azimio."
Jukumu la NATO
Kuhusu ulinzi, Katibu Mkuu wa NATO Mark Rutte alimfikia Rais Donald Trump kwa simu: Tunafanyia kazi usalama wa Aktiki na Greenland,” huku rais wa Marekani akitangaza kwenye mitandao ya kijamii: “Kwa miaka 20, NATO imekuwa ikiiambia Denmark kwamba tishio la Urusi lazima liondolewe kutoka Greenland; kwa bahati mbaya, Copenhagen haijaweza kufanya hivyo. Sasa ni wakati, na tutafanya hivyo.”
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here