"Mungu ni sherehe."Kugundua Furaha ya Kikristo,ni kitabu kipya cha Sylvain Detoc
Vatican News.
Katika Kitabu kipya chenye Kichwa Mungu ni sherehe : kugundua Furaha ya Ukristo, Mwandishi anaeleza kwamba "Furaha kubwa ya Injili si chaguo kwa baadhi ya 'wapenzi wa tukio la kuzaliwa kwa Yesu.' Ni hali ya kawaida labda si ya kawaida sana, ole!' maisha ya Kikristo." Sylvain Detoc anaamini kuwa: Wakristo wana nyuso ndefu sana, hawachukui mwaliko wa Yesu wa kusherehekea kwa uzito (!) Kwa sababu, ndani mwao kabisa, wengi wana imani: "Mwenye kujaribu ni mlaghai stadi. Amekuwa akijaribu kutuweka katika udanganyifu tangu wakati wa dhambi ya asili: angetufanya tuamini kwamba dhambi ni sherehe, na utakatifu ni adhabu."
Kusherehekea katika Maandiko
Marejeo ya Nietzsche na wenzake ni wazi: "Wokovu wa milele ungekuwa thawabu ya maisha yaliyotumika duniani katika uchovu wa kibinadamu." Hakuna hata moja kati ya haya, anasema mwandishi, ambaye, kama mtaalamu wa Mababa wa Kanisa, anajua vyema thamani ya mwili katika imani ya Kikristo: "Tunawezaje kuweka tumaini letu kwa Mungu ikiwa tunamshuku kuwa anatunyima furaha na ikiwa Ukristo unaonekana kama hotuba ya maadili tu inayokataza kila kitu kinachoonekana kutamanika?"
Jibu linaonekana wazi katika kurasa hizi: "Kusherehekea, kula, kunywa, kucheza, kuimba, kuruka: Maandiko hayangezingatia sana furaha hizi zote zinazowafanya wanadamu watetemeke ikiwa hayangeweza kusemwa kuwahusu, kama ilivyo katika wimbo wa Uumbaji: 'Mambo haya ni mazuri sana.'" Kitabu cha Mungu ni sherehe: kugundua Furaha ya Ukristo kilichoandikwa na Mdominikani wa Kifaransa, Sylvain Detoc, kinapatikana katika maduka ya vitabu ya Vatican (LEV) kuanzia tarehe 11 Februari (chenye kurasa 160, kinauzwa Euro 14)
Mwandishi
Sylvain Detoc (1979), mtawa wa Dominikani mwenye shahada ya uzamivu katika fasihi na taalimungu, alifundisha fasihi katika Sorbonne huko Paris na Chuo Kikuu Katoliki cha Lyon. Anafundisha Taalimungu ya Mababa katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Mtakatifu Thomas Aquinas – Angelicum, Roma, katika Taasisi Kikatoliki, na katika Chuo Kikuu cha Dominikan huko Toulouse, ambapo pia anahudumu kama Padre wa Chuo kikuu. Yeye ni mjumbe wa bodi ya wahariri ya Revue Thomiste. Alichapisha Utukufu wa Wema Bila Malipo (2024) na Nyumba ya Viatabu ya Vatican(LEV):
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku: Just click here