Papa atembelea Kituo cha Afya na kutoa faraja kwa wagonjwa
Vatican News
Baada ya umati wa watu katika Misa kwenye Uwanja wa Japoma wa Douala, Ijumaa tarehe 17 Aprili 2026, Baba Mtakatifu Leo XIV aliwatembelea wagonjwa katika Hospitali Katoliki ya Mtakatifu Paulo, ambapo aliwapa mabembelezo na faraja. Akifuatana na mkurugenzi wa Hospitali hiyo, alitembelea Wodi kadhaa. Kituo hicho, kinachosimamiwa na Jimbo Kuu la Douala, kiko katika wilaya ya Bassa. Kulikuwa na muda wa kutafakari katika Kikanisa, na Papa Leo XIV, alisimama katika uwanja wa ndani na kuwasalimia wafanyakazi na baadhi ya wagonjwa kwa ufupi.
Ishara ya Faraja
“Kila siku, bila usumbufu, tunajitahidi kutoa huduma ya afya inayopatikana kwa urahisi na ubora. Uangalifu maalum hutolewa kwa wanawake,” alisema Mkurugenzi wa Kituo hicho. Baadhi ya wagonjwa hao waliweza kumpatia mkono Baba Mtakatifu, ambaye, kwa huruma isiyo na kikomo, alikubali mateso ya watoto na watu wazima. Baraka zake zilitolewa kwa kila mtu, ikiwa ni pamoja na wanafamilia waliokuwepo, kabla ya kumsalimia kila mgonjwa mmoja mmoja.
Majeraha ya Nafsi na Mwili
Baada ya Sala ya Malkia wa Mbingu, Baba Mtakatifu Leo XIV aliweza kuingia vyumba ambavyo baadhi ya wagonjwa wanatunzwa. Alikaribia watoto na wazee. Mwishoni mwa ziara hiyo, muda mfupi kabla ya saa 8 alasiri saa zahuko, Papa Leo XIV aliondoka kwenda uwanja wa ndege kwa ajili ya kurudi kwake Yaounde, ambapo alitakiwa kukutana na wanafunzi na wasomi wa Chuo Kikuu Katoliki cha Afrika ya Kati. Kwa hivyo “uwepo wa Mrithi unagusa majeraha ya vita na yale ya mwili, ukificha majeraha makubwa, ukiomba uponyaji kwa roho na mwili.”
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.
