Kuanzia Pompei hadi Lampedusa,ni Ratiba ya Kichungaji ya Papa Leo XIV,Italia
Vatican News
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Habari ya Vatican ilitangaza, Aprili 25, mipango ya ziara za kichungaji za Papa Leo XIV nchini Italia, kuanzia huko Pompei, Napoli, Acerra, Pavia, Mtakatifu Angelo Lodigiano na Lampedusa. Papa atasafiri hadi Pompeii na Napoli mnamo Mei 8 ili kusali mbele ya mabaki ya Mtakatifu Bartolo Longo, mwanzilishi wa Madhabahu ya Bikira Maria wa Rozari Takatifu, kuongoza Misa na pia sala kwa Mama Yetu, na pia kukutana na Kanisa na raia wa mji mkuu wa Mkoa wa Campagna, kama ilivyotangazwa Aprili 24 kwenye madhabahu na Jimbo Kuu la Napoli
Katika “Ardhi ya Moto”
Mnamo Mei 23, Papa atawatembelea watu wa eneo liitwalo, "Ardhi ya Moto" huko Acerra. Safari hiyo imepangwa kuwasili kwa helikopta saa 2:45 asubuhi katika uwanja wa michezo wa "Arcoleo." Akikaribishwa na Askofu Antonio Di Donna, Meya Tito d'Errico, Mkuu wa Mkoa wa Campagna Roberto Fico, na Mkuu wa Napoli Michele Di Bari, Papa atawasili katika Kanisa kuu saa 9. 15 asubuhi. Watakao msuburi ni Maaskofu wa Mkoa wa Campania, mapadre, watawa, na familia za wale waliokufa kutokana na uchafuzi wa mazingira. Saa 4:30 asubuhi, huko Uwanja wa Calipari, atakutana na mameya na waamini wa manispaa mbalimbali za "Ardhi ya Moto." Papa pia atatoa hotuba hapo, kabla ya kurudi Vatican.
Juni 20 huko Pavia na Mtakatifu Angelo Lodigiano
Safari ya Papa Leo XIV ya kwenda Lombardia mnamo Juni 20 inajumuisha vituo viwili: Pavia na Mtakatifu Angelo Lodigiano. Papa Leo XIV ataondoka kwa helikopta kutoka kituo cha helikopta cha Vatican saa 1:00 asubuhi na kutua saa 2:45 asubuhi katika Uwanja wa Raga wa CUS huko Cravino, ambapo atakaribishwa na mamlaka za kiraia na kidini. Kisha atahamishiwa kwa gari hadi Kituo cha Kitaifa cha Tiba ya Saratani (CNAO), ambapo Papa atakutana na mameneja, wafanyakazi wa matibabu, na, pamoja na wazazi wao, baadhi ya watoto wanaopatiwa matibabu. Saa 3:30 asubuhi, ataondoka kwenda Basilika ya Mtakatifu Petro huko Ciel d'Oro, ambapo mabaki ya Mtakatifu Agostino yamehifadhiwa.
Papa atakaribishwa na ndugu zake wa Shirika lake: Padre Joseph L. Farrell, Mkuu wa Shirika la Mtakatifu Agostino; Padre Gabriele Pedicino, Mkuu wa Kanda la Kiagostinian nchini Italia; na Padre Gianfranco Casagrande, Mkuu wa Conventi ya Watawa aliyekabidhiwa uchungaji wa Basilika ya Mtakatifu Petro huko Ciel d'Oro. Mkutano mfupi na Jumuiya ya Kiagostiniani, utafuatiwa na salamu kwa Maaskofu wa Lombardia na baadhi ya washirika wao. Saa 4:15 asubuhi, Papa Leo XIV ataongoza Ibada ya Neno la Mungu katika Basilika, ikifuatiwa na kuheshimiwa kwa masalia ya Askofu wa Hippo.
Papa atatoa hotuba na kisha, saa 5. 00 asubuhi, atahamia Kanisa kuu, ambapo watoto wataweka heshima ya maua katika uwanja wa Kanisa na salamu kwao na kwa Jumuiya ya Amerika Kusini. Kisha Papa Leo XIV ataingia katika Kanisa kuu na, akikaribishwa humo atakaa humo kwa kuabudu Sakramenti Takatifu na mbele ya madhabahu ya Mtakatifu Siro, Askofu wa kwanza na Mtakatifu mlinzi wa Jimbo na Jiji. Baada ya hapo, Papa atatembea hadi Uwanja wa Vittoria kwa ajili ya mkutano na raia saa 11:30 jioni.
Baada ya hotuba na salamu, safari itaendelea hadi Uwanja wa Raga wa CUS huko Cravino, ambapo saa 12:45 jioni, helikopta itaondoka kwenda Mtakatifu Angelo Lodigiano, ambapo atatoa hotuba katika Parokia ya Watakatifu Anthoni Abate na Francesca Cabrini. Saa 1:30 jioni, baada ya kuondoka Parokiani, Papa Leo XIV ataelekea Uwanja wa Manispaa kuwaaga viongozi na kuondoka kuelekea kituo cha helikopta cha Vatican, akiwasili saa 3:15 usiku.
Ziara ya Lampedusa Julai 4
Hatimaye, Lampedusa anamsubiri Papa Julai 4. Papa Leo XIV atafika kisiwa cha Sicilia kwa ndege, akiondoka kutoka Uwanja wa Ndege wa Ciampino saa 1:45 asubuhi. Baada ya kutua saa 3.00 asubuhi, Papa Leo XIV atasimama kwanza kwenye makaburi, ambapo ataweka heshima ya maua kwenye makaburi, kisha kwenye "Lango la Ulaya," na kisha Molo Favaloro, kwa ajili ya baraka ya bamba la kumkumbuka Papa Francisko na salamu kwa wahamiaji kadhaa.
Misa imepangwa kufanyika saa 4:30 asubuhi. Baada ya hapo, baada ya kuwasalimia maafisa, watoto, wagonjwa, na watu wa kujitolea, Papa ataelekea uwanja wa ndege kwa ajili ya kuondoka saa 6:30 mchana. Amepangwa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Ciampino saa 7:45 mchana, ambapo atarudi mjini Vatican.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.
