Ujumbe wa Papa kwa Maaskofu wa Ufaransa:inahitajika uvumilivu katika kutetea elimu Katoliki
Na Angella Rwezaula - Vatican.
Katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kipindi cha kuchanua wa Maaskofu wa Ufaransa uliofunguliwa Machi 24 hadi 26, walitumiwa ujumbe kutoka kwa Papa Leo XIV, uliosainiwa na Katibu Mkuu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin. Elimu, unyanyasaji na liturujia vinaunda mada kuu tatu za barua iliyotumwa kwa Maaskofu hao. Mada hizi hizo zitaongoza majadiliano yao kwa siku nne katika Madhabahu ya Kitaifa na Kimataifa ya Maria huko Lourdes. Huku kukiwa na wasiwasi unaoendelea wa umma kuhusu kashfa za hivi karibuni za nyanyaso katika taasisi za elimu, Baba Mtakatifu Leo XIV alieleza mazingira ya uadui unaoongezeka, lakini akihimiza uvumilivu katika kutetea elimu Katoliki. Papa, alitoa wito wa utambulisho wake wa Kikristo, sababu yake halisi ilindwe kwa dhamira, huku wakiendelea kukuza uwazi na heshima kwa imani za wote.
Kusikiliza kilio cha kimya kimya
Suala la pili ambalo Maaskofu wanashughulikia ni suala la nyanyaso za watoto. Kanisa nchini Ufaransa limefanya juhudi endelevu za kukabiliana na mgogoro huo, hasa tangu kuundwa kwa Tume Huru ya Unyanyasaji wa Kijinsia Kanisani (CIASE) mnamo tarehe 8 Februari 2019, Juma chache kabla ya mkutano wa Vatican ulioitishwa na Papa Francisko. Katika mkutano huo, Papa Francisko alisisitiza “wajibu wa Kanisa kusikiliza kwa makini” “kilio cha kimya kimya” cha waathiriwa. Papa Leo XIV akirudia hilo, aliwataka Maaskofu wa Ufaransa kuendelea kuwasikiliza na kuwajali waathiriwa, huku akisisitiza hitaji la hatua za kinga za muda mrefu na kutoa huruma ya Mungu kwa wote.
Katika hatua hii, Papa Leo XIV aliongeza kwamba "mapadre walio na hatia ya unyanyasaji hawapaswi kutengwa na huruma hiyo, lakini wanapaswa kuwa mada ya tafakari yao ya kichungaji." Wakati huo huo, aliwapa Maaskofu maneno ya kutia moyo na kufufua imani yake kwao, akibainisha kwamba wengi "wameathiriwa sana" na matokeo ya unyanyasaji uliofanywa na baadhi ya mapadre wenzao.
Suala la Ibada ya kiutamaduni ya Vetus Ordo ya kilatini
Hatimaye, Papa alizungumzia suala ambalo anazingatia sana kuhusu idadi inayoongezeka ya jumuiya zilizounganishwa na Vetus Ordo (yaani ya sherehe ya Misa ya Kilatini kulingana na liturujia iliyotumika kabla ya Mtaguso wa Pili wa Vatican). Katika suala hilo Papa Leo XIV alionesha wasiwasi kwamba hali hii inaweza kufungua "jeraha chungu ndani ya Kanisa kuhusu sherehe ya Misa," ambayo aliielezea kama "sakramenti ya umoja." Ikiwa Kanisa ni mama anayewajali watoto wake, alisema, lazima aponye majeraha na ajifunze kuwatazama wengine "kwa uelewa mpya na usikivu zaidi."
Maaskofu watafute suluhisho kwa msaada wa Roho Mtakatifu
Kwa hivyo aliwaalika Maaskofu, kwa msaada wa Roho Mtakatifu, kutafuta "suluhisho thabiti" ambazo zitawajumuisha kwa ukarimu wale walioshikamana kwa dhati na Vetus Ordo, huku wakibaki waaminifu kwa maelekezo ya Mtaguso wa Pili wa Vatican. Kwa kutambua "nyakati ngumu" zinazokabili Kanisa, Papa Leo XIV pia alielekeza kwenye "ishara za matumaini na uwepo wa Mungu mioyoni mwa watu." Ishara moja kama hiyo ni ongezeko kubwa la idadi ya wakatekumeni katika kipindi cha miaka kumi iliyopita.
Kuongezeka kwa wabatizwa wapya Ufaransa
Idadi ya wagombea watakaopokea ubatizo katika Mkesha wa Pasaka tarehe 4 Aprili 2026 itatangazwa hivi karibuni na Baraza la Maaskofu wa Ufaransa, lakini mwelekeo wa kupanda unaonekana kuendelea hadi 2026. Kulikuwa na wakatekumeni 17,800 mwaka 2025, na idadi hiyo inaweza kuzidi 20,000 mwaka huu. Hii inaonesha shauku mpya ya kiroho, ingawa ni lazima ionekane katika muktadha mpana wa zaidi ya miongo miwili ya maombi ya ubatizo yaliyopungua.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku:Just click here.
