2026.02.08 Huduma ya maua na ujenzi. 2026.02.08 Huduma ya maua na ujenzi.  (@VATICAN MEDIA )

Papa Leo XIV awashukuru Wapambaji na Ofisi ya Ujenzi kwa huduma ya busara na thamani

Papa Leo aliwaaka kuungana naye kuwafikiria wale wanaopita katika maeneo wayohudumia na kuwaombea.Hakika,imani na sala hutoa maana kamili kwa kila kitu wanachofanya.Alisema hayo alipokutana mjini Vatican na Wasimamizi na Wafanyakazi wa Ofisi ya Maua na Ujenzi wa Jiji la Vatican,Dominika tarehe 8 Februari 2026,kabla ya Sala ya Malaika.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Dominika tarehe 8 Februari 2026, Baba Mtakatifu Leo XIV alikutana mjini Vaticanna Wasimamizi na Wafanyakazi wa Ofisi ya Mau na Ujenzi. Katika hotuba yake  awali ya yote alianza na ishara ya Msalaba: “Kwa jina la Baba na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amani iwe nanyi! Habari za asubuhi! Dominika njema na karibu! Kaka na dada wapendwa wa Wataalamu wa Maua na Idara ya Ujenzi, pamoja na familia zenu. Pia kuna wimbo unaotusindikiza, na ni mzuri sana... Na muendelee kuimba.” Papa alianza hivyo na kuendelea kuonesha alivyotaka kukutana nao kabla ya sala na baadaye kushiriki pamoja katika sala ya Malaika wa Bwana na waamini wote ambao walikuwa tayari wameanza kukusanyika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro. Awali ya yote alikuwa na utashi wa kuwasalimia na kuwashukuru kwa kazi yao wanayofanya kwa bidii sasa. Kama wakuu, wafanyakazi na wataalamu katika sekta hiyo ya Mji wa Vatican, wamejipambanua kwa ari kubwa ya shughuli zao, hasa wakati wa mwaka wa Jubilei ambayo imehitimishwa hivi karibuni.

Papa Leo na Wahudumu Vatican
Papa Leo na Wahudumu Vatican   (@VATICAN MEDIA)

Shukrani hata kwa jitihada ya pamoja, mamilioni ya wanahija waliwezza kusihi kwa utaratibu, na utulivu wa njia ya kuelekea Mlango Mtakatifu, wakishirikimatunda mema katika maadhimisho ya kiliturujia, Katekesi na matukio mengine. Ni shukrani ambayo aliitoa kutoka moyoni mwake, na kwamba "inageuka kuwa mwamko kwa ajili ya mipango ijayo, ambayo inatazama,  iwe kwa kusasisha kila wakati huduma za kiufundi na uendeshaji,  na ile ya umakini wa utunzaji wa mazingira mjini Vatican, hasa kwenye nafasi za  sala na katika mikutano na Papa."  Kupamba sehemu na usalama wa majengo vinapata kiukweli maana yake ya juu zaidi katika kusaidia ibada inayotolewa kwa waamini na huduma ya kichungaji ya Makanisa.

Papa na Wahudumu wa maua na ujenzi Vatican
Papa na Wahudumu wa maua na ujenzi Vatican   (@VATICAN MEDIA)

Kwa namna ya pekee, katika Basilika ya Mtakatifu Petro ni mahali patakatifu ambapo panahitaji kulindwa hasa kama hekalu la kutafakari, kwa sala, na maajabu ya kiroho. Uwanja ambao unakumbatia ulimwengu kwa nguzo zake za kushangaza, ni “tiketi ya kuingia” kwa namna ya kuelezea, ya kukaribisha wote. Baba Mtakatifu kwa namna hiyo aliwaalika wakati wanajikita na shughuli za kazi zao za kila siku, kwamba ni ya busara na yenye thamani kwa utume wa Kitume wa Papa. Kiukweli ni sehemu ya shughuli tata za Gavana na Kurugenzi ya Miundombinu ya mji wa Vatican na huduma, ambazo “ninazipongeza kwa usimamizi wao wa bidii wa kazi nyingi ndani ya Vatican.

Kila mmoja kwa upande wake, hasa wakati wa majaribu, Papa alisema, "tukumbuke kwamba sisi ni viungo vya kiumbe kimoja, ambacho kusudi lake ni kushuhudia Injili kulingana na amri ya Bwana, Mchungaji Mwema na Kichwa cha Kanisa. Kama ishara ya shukrani zangu, nawabariki kwa moyo wote, familia zenu zinazowasindikiza leo, na kazi yenu. Asante sana.

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku: Just click here.

08 Februari 2026, 11:34