Papa Leo XIV akutana na Waziri Mkuu wa Cabo Verde
Vatican News
Jumamosi tarehe 14 Februari 2026, Baba. Mtakatifu Leo XIV alimpokea na kuzungumza na José Ulisses Correia na Silva, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Cabo Verde, katika Jumba la kitume, Vatican. Hii iliripotiwa katika taarifa kutoka Ofisi ya Vyombo vya Habari ya Vatican.
Mwishoni mwa mkutano huo, Waziri Mkuu huyo alikutana na Kardinali Pietro Parolin, akifuatana na Monsinyo Mihăiţă Blaj, Katibu Msaidizi wa Vatican wa Mahusiano na Mashirika ya Kimataifa.
"Wakati wa majadiliano ya kirafiki," maandishi yanasema, "hali chanya ya uhusiano kati ya Vatican na Jamhuri ya Cabo Verde ilithibitishwa tena, hasa ikimaanisha mchango wa Kanisa Katoliki nchini humo na utekelezaji wa makubaliano ya pande mbili yaliyoidhinishwa mwaka 2014."
Mkutano huo pia ulizungumzia baadhi ya vipengele vya hali ya kijamii na kiuchumi kitaifa. Pia walibadilishana maoni kuhusu masuala ya sasa ya kikanda, hasa masuala ya usalama katika eneo la Afrika Magharibi.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here
