2023.04.18 Mons. Anthony Onyemuche Ekpo,Katibu msaidizi wa Baraza la Kipapa la Maendeleo Frungamani ya Binadamu ameteuliwa na Papa kuwa Mtadhimini Mkuu wa Vatican. 2023.04.18 Mons. Anthony Onyemuche Ekpo,Katibu msaidizi wa Baraza la Kipapa la Maendeleo Frungamani ya Binadamu ameteuliwa na Papa kuwa Mtadhimini Mkuu wa Vatican. 

Papa Leo XIV amteua Monsinyo Ekpo kuwa Mtathmini mpya wa Vatican

Papa Leo XIV amemchagua Mtaalimungu mwenye miaka 44 mzaliwa wa Nigeria,ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Katibu Msaidizi wa Baraza la Kipapa la Kuhamasisha Maendeleo Fungamani ya Binadamu kuwa Mtathimini mpya wa Vatican.Aliwahi kufanya kazi katika Kitengo cha Masuala ya Jumla ya Sekretarieti ya Vatica.Pia Papa amemteua Katibu msaidizi mpya wa Kitengo cha Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa pia Mons.Mihăiţă Blaj.

Na Salvatore Cernuzio – Vatican.

Ni Kijana mwenye asili ya Nigeria. Kufuatia uteuzi wa hivi karibuni wa Padre Edward Daniang Daleng, Mwanashirika wa Shirika la Mtakatifu Agostino,O.S.A., kuwa Makamu Mkuu mpya wa Nyumba ya Kipapa,  Baba Mtakatifu Leo XIV amemteua Padre mwingine kutoka Bara la Afrika kuwa katika nafasi muhimu ya Curia Romana(Baraza la Wawakilishi la Roma): Monsinyo Anthony Onyemuche Ekpo, tarehe 19 Novemba 2025, kuwa Mtathmini mpya wa Masuala ya Jumla ya Sekretarieti ya Vatican, sehemu ambayo alikuwa amehudumu karibu miaka sita kabla ya Papa Francisko kumteua kuwa Katibu Msaidizi wa Baraza la Kipapa la Kuhamasisha Maendeleo Fungamani ya Binadamu.

Il cardinale Parolin saluta il nuovo assessore

Kardinali  Parolin akimsalimia na kumkabidhi barua Mtathimini mpya wa Vatican.

Hadi uteuzi alikuwa Katibu Msaidizi wa Baraza la Kipapa la Maendeleo Fungamani ya Binadamu

Padre huyo alizaliwa Umudike nchini Nigeria, mnamo 1981, na  kupewa daraja la Upadre mwaka 2011 na kuteuliwa kuwa Msimamizi wa Kikanisa cha Baba Mtakatifu  mnamo Machi 2023. Mafunzo yake ni kwamba alipata Shahada ya Uzamivu katika Taalimungu  ya Kimfumo kutoka Chuo Kikuu Katoliki cha Australia mnamo 2013, na Shahada ya Uzamivu katika Sheria ya Kanisa kutoka Chuo Kikuu cha Gregorian Roma mnamo 2021. Alijiung katika huduma ya Vatican kama Afisa wa Kitengo cha Masuala ya Jumla mnamo tarehe 5 Septemba 2016. Mnamo Aprili 2023, aliteuliwa kuwa Katibu Msaidizi wa Baraza la Kipapa la Kuhamasisha Maendeleo Fungamani ya Binadamu, akisaidiana  katika kazi ya Mwenyekiti wa Baraza la kipapa hilo, Kardinali Michael Czerny, pamoja na Katibu Mkuu Sr Alessandra Smerilli, na katibu mwingine msaidizi, Kardinali Fabio Baggio.

"Hamu yangu ni kuweza kushirikiana na wakubwa na wafanyakazi wa Baraza la Kipapa ili kuendeleza maono ya Baraza la Kipapa na utume wa Kanisa." Ekpo alisema hayo wakati huo katika siku ya uteuzi wake, akiwaaga viongozi na wafanyakazi wenzake, ambao aliwashukuru "kwa urafiki wao na kazi yao ya pamoja katika miaka hii," na akaomba kwamba Mungu ampatie "neema ya kutekeleza, kwa furaha, shauku, na kujitolea" huduma yake kwa Kanisa.

Monsinyo Ekpo anamrithi Monsinyo Roberto Campisi, aliyeteuliwa kunako tarehe 27 Septemba 2025 kuwa Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican kwa UNESCO, akiwa na jukumu la pia kusimamia shughuli za Mashirika ya Kikatoliki ya Kimataifa. Kwa njia hiyo Mtathmini mpya anazungumza lugha nne: mbali na Kiingereza, Kiitaliano, na Kifaransa, pia anazungumza Igbo, lugha ya asili ya nchi yake.

La comunicazione delle nomine nella Biblioteca della Segreteria di Stato

Wakati wa kuwatangaza viongozi wapya katika Maktaba ya Katibu Mkuu wa Vatican.

Katibu Mpya Msaidizi wa Kitengo cha Mahusiano na Mataifa

Wakati huo huo, Ofisi ya Habari ya Vatican ilitangaza uteuzi mwingine katika Sekretarieti ya Vatican: ile ya  wa Monsinyo Mihăiţă Blaj kuwa Katibu Mpya Msaidizi wa Vatican katika  Kitengo cha Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.

Wasifu wake

Mromania aliyezaliwa Gherăeşti mnamo 1978, Monsi Mihăiţă Blaj, hapo awali alikuwa Mshauri wa Ubalozi huku akihudumu katika Kitengo hicho hicho. Alipewa daraja la Upadre  mnamo tarehe 29  Juni 2004; akapewa kwa ajili ya Jimbo la Iaşi, Romania; mhitimu wa Taalimungu; alijiunga katika Huduma ya Kidiplomasia ya Vatican mnamo tarehe 1 Julai 2012, na alitumwa katika  Ubalozi wa  Vatican  huko Ecuador,  kama Mshirika; akahamishiwa Ubalozi wa Vatican huko Georgia mnamo tarehe 1  Julai 2015; akahamishiwa  tena Ubalozi wa Vatican huko Chad mnamo  tarehe 5 Januari 2019; Alihamishiwa kwenye Kitengo cha Sekretarieti ya Vatican cha Mahusiano Nchi na Mashirika ya Kimataifa mnamo tarehe 4 Januari 2022. Anazungumza Kiitaliano, Kifaransa, Kiingereza, Kihispania, na Kijerumani

 Il saluto del segretario di Stato al nuovo sottosegretario per la Sezione per i Rapporti con gli Stati, monsignor Blaj

Kardinali Parolin Katibu wa Vatican akumkabidhi Mons. Blaj, Katibu Mpya Msaidizi wa Kitengo cha Mahusiano na Nchi na Mashirika ya Kimataifa.

Utuezi wa baadhi ya nafasi za Curia Romana

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here

 

19 Novemba 2025, 13:11