2025.09.12 Papa akutana na Rais wa Jamhuri ya Moldavia Bi Maia Sandu. 2025.09.12 Papa akutana na Rais wa Jamhuri ya Moldavia Bi Maia Sandu.  (@VATICAN MEDIA)

Papa Leo XIV akutana na Rais wa Moldavia

Baba Mtakatifu Leo XIV,Ijumaa Septeba 2025,alikutana na Bi Maia Sandu katika Jumba la Kitume mjini vatican.Majadiliano katika Sekretarieti ya Vatican yalilenga juu ya hali ya amani na usalama ya kikanda na kimataifa,kwa kuzingatia hasa maendeleo ya hivi karibuni nchini Ukraine.

Vatican News

Ijumaa asubuhi  tarehe 12 Septemba 2025, Baba Mtakatifu  Leo XIV alikutana na Bi Maia Sandu, Rais wa Jamhuri ya Moldovia, katika Jumba la Kitume, mjini Vatican.

Rais wa Moldavia akizungumza na Papa Leo XIV
Rais wa Moldavia akizungumza na Papa Leo XIV   (@VATICAN MEDIA)

Baada ya Mkutano huo na Papa pia  alikutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican, akifuatana na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.

Wakati wa kubadilishana zawadi
Wakati wa kubadilishana zawadi   (@VATICAN MEDIA)

Majadiliano katika Sekretarieti ya Nchi

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Waandishi wa Habari Vatican, ilibainisha, "Wakati wa mkutano wa kidugu katika Sekretarieti ya Vatican, shukrani ilioneshwa kwa uhusiano mzuri uliopo baina ya nchi mbili, kwa matumaini ya kuimarishwa zaidi." Kadhalika, majadiliano yalilenga juu ya hali ya amani na usalama katika ngazi mahalia, kikanda na kimataifa, kwa kuzingatia hasa  hali inavyoendelea ya hivi karibuni nchini Ukraine.

12 Septemba 2025, 16:39