2025.09.16 Parokia ya Familia Takatifu katika mji  Gaza. 2025.09.16 Parokia ya Familia Takatifu katika mji Gaza. 

Papa ampigia simu Paroko wa Gaza

Paroko wa Familia Takatifu alishuhudia nguvu ya sala kwa vyombo vya habari vya Vatican wakati mashambulizi ya Israeli yanapoendelea."Hakuna mahali palipo salama. Idadi ya milipuko ya mabomu inaongezeka kila siku na kila siku idadi ya uharibifu,vifo,kupotea chini ya vifusi na waliojeruhiwa inaongezeka."

Francesca Sabatinelli – Vatican.

Janga la vita hii lisiloisha ni kwamba inakuwa mbaya zaidi kila siku. Kukabiliwa na hali ya kutokuwa na msaada husababisha maumivu makubwa, lakini maombi na baraka za Mungu ni msaada wetu. Baada ya usiku wa kutisha ulioadhimishwa na mashambulizi ya Israel huko Gaza, maneno ya Padre Gabriel Romanelli, Paroko wa Familia Takatifu katika Jiji la Gaza, alisistiza kuwa licha ya kile kinachoendelea "tunabaki kujawa na matumaini, alama ya ubinadamu na huruma, na kuomba kwa ajili ya uhuru na yote tunayainua  katika madhabahu ya Gaza, madhabahu ya amani, ambapo sisi tunainua Sakramenti Takatifu kila siku.” Padre Romanelli, alisema hayo akizungumza na vyombo vya habari vya Vatican, kwamba  Uhuru, kwa  Wapalestina, kwa Waisraeli, kwa mateka,  na kwa wale wote  walionyiwa, acha vita vikome, ili watu wanaoishi katika Ukanda wa Gaza wapate vitu muhimu vya kuishi, na sio kuishi, lakini kuishi, kujenga upya maisha yao."

Wasiwasi kwa watu wa Gaza

Mwandishi wa habari jini tarehe 16 Septemba wakati papa Leo XIV anatoka huko Castel Gandolfi alisikika akiuliza: Kuhama kwa  watu huko Gaza, umeona wangapi wanakimbia...?" Papa ali thibitisha kuwa alizungumza kwa njia ya simu na Jumuiya ya Gaza na Padre wa parokia hiyo na kueleza hofu yake. "Wengi," alisema, "hawana pa kwenda, na hivyo ni jambo la kuhangaisha. Pia nilizungumza na watu wetu huko, pamoja na  Padre wa Parokia. Kwa sasa, wanataka kubaki; bado wanapinga, lakini kiukweli tunahitaji kutafuta suluhisho lingine."


Mgogoro wa Gaza

Padre Romanelli,  kutokana na shuhuda na taarifa zilizokusanywa, alifanikiwa kuona ramani ya operesheni ya kijeshi, ambayo inaonekana kugonga hasa ​​maeneo ya magharibi na kaskazini-magharibi ya Jiji la Gaza na kwa kiasi fulani kusini, kuwa sio mashariki mwa jiji, ambapo parokia hiyo iko, katika sehemu ya zamani ya jiji, katika kitongoji cha Zeitoun. Sauti ya silaha pia zinafika huko, japokuwa wakati wingine zinasikika kwa mbali kwamba: "Hakuna milipuko ya mabomu karibu nasi kwa wakati huu." Sio kali kama mlipuko ambao saa chache mapema ulikatiza maombi ya waamini waliokusanyika kanisani. Picha zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii na Padre Romanelli mwenyewe zilisambaa sana, zikionesha waamini, wakitikiswa na kelele, wakisalia kukumbukwa.

"Huo ndio ukweli. Sisi, tulio kwenye Kalvari hii ya Gaza, tunaomba amani na haki kwa wote. Na tunaendelea kuomba; hii ndiyo misheni yetu. Bwana alitufundisha kuhubiri, kumwamini, na kumtumaini Yeye. Bila shaka, kuna mateso, lakini tuna mengi ya kumshukuru Mungu." Kama baraka ya ndoa kati ya vijana wawili Wakristo; kama ubatizo wa mtoto aitwaye Marco, mdogo wa wakimbizi; kama baraka za uwasilishaji, katika siku za hivi karibuni, kwa "watu 65, ikiwa ni pamoja na watoto, vijana, vijana, na watu wazima, ya scapular ya Bikira Mtakatifu zaidi kama ishara ya ulinzi na baraka."

Uharibifu na Mauti

Ni vigumu kufikiria ni wangapi hadi sasa wameondoka ili kuepuka milipuko ya mabomu. "Kila mtu ninashuhudia kwamba mashambulizi pia yanafanyika kusini. Hakuna mahali salama. Idadi ya milipuko ya mabomu inaongezeka kila siku, na kila siku idadi ya uharibifu, vifo, wale wanaopotea chini ya vifusi, na waliojeruhiwa huongezeka." Romanelli, na wale wote wanaofanya kazi naye katika parokia hiyo, wanaendelea kusaidia wakimbizi 450 katika kanisa, "hasa ​​wazee; wagonjwa, familia zilizo na watoto wadogo, na kisha wasiolala, watoto wa Mama Teresa, ambao wamekuwa wakiishi nasi tangu kabla ya vita. Tunasambaza tulichonacho, chakula na maji. Baadhi ya majirani zetu wameondoka kuelekea kusini, lakini maeneo mengi ya jirani yamebaki hapa. Hali inazidi kuwa mbaya zaidi kila siku, na hakuna anayejua itafikia wapi au siku zijazo ni nini."

17 Septemba 2025, 08:23