Utawala wa Trump wapunguza Ufadhili kwa Mashirika ya Kikatoliki Kusini mwa Florida. Utawala wa Trump wapunguza Ufadhili kwa Mashirika ya Kikatoliki Kusini mwa Florida.  (2026 Getty Images)

Marekani:Askofu Mkuu Wenski asikitishwa kupunguzwa kwa misaada ya Watoto Marekani

Baada ya serikali ya Marekani kupunguzwa kwa ufadhili kwa ajili ya Caritas,Askofu Mkuu Thomas Wenski wa Jimbo Kuu la Miami alilaani tendo hilo na kusema kwamba huduma zinazotolewa na Kanisa Katoliki kwa watoto wasio na walezi zitalazimika kufungwa.

Na Deborah Castellano Lubov – Vatican.

"Kwa zaidi ya miaka 60, huduma za Jimbo Kuu  Katoliki la Miami kwa watoto wasio na walezi zimetambuliwa kwa ubora wao na zimetumika kama mfano kwa mashirika mengine  nchini kote. Rekodi yetu ya kufuatilia katika kuwahudumia watu walio hatarini hailinganishwi. Hata hivyo, huduma za Kanisa Kuu la Miami kwa watoto wasio na walezi, ufadhili wao na serikali umesitishwa na hivyo zitalazimika kufungwa ndani ya miezi mitatu." Haya ni kutoka katika taarifa kwenye tovuti ya Jimbo Kuu la Miami, ya Askofu Mkuu Thomas Wenski akilaani uamuzi wa serikali ya Marekani wa kupunguza msaada wa Shirika la Huduma ya upendo (Caritas) na kukatisha uhusiano wa zaidi ya miaka 60 na Shirika la Misaada la Katoliki katika Jimbo Kuu la Miami.

Watoto 14,000 kutoka nchini  Cuba waliotumwa peke yao kutoka Cuba

Askofu Mkuu alikumbuka kwamba ushirikiano ulianza na Operesheni "Pedro Pan," ambayo ilianza chini ya uongozi wa Padre kijana wa Ireland wa wakati huo, akiwepo Askofu Bryan O. Walsh, ambaye alisaidia kuwapatia makazi mapya watoto wapatao 14,000 kutoka nchini Cuba waliotumwa peke yao nchini humo na wazazi waliokata tamaa wakitaka kuwaepusha kutokana na mafundisho ya kikomunisti. Askofu Mkuu Wenski alibainisha kuwa kuanzia mwaka 1960 hadi sasa, Jimbo Kuu limefanya kazi kwa ukaribu sana na Ofisi ya Makazi ya Wakimbizi ili kutoa makazi na huduma zingine kwa maelfu ya watoto wadogo wasio na wazazi wa mataifa yote.

Matokeo chanya ya ushirikiano

Alibainisha kuwa leo, kituo kinachoitwa Kijiji cha Watoto cha Padre Bryan O. Walsh huko Pwani  ya Palmetto kinaweza kuwapatia makazi watoto hadi 81. Programu hiyo husaidia kuwaweka watoto katika malezi ya watoto, kuwaunganisha tena na wanafamilia, na kutoa huduma za usaidizi. Alibainisha kuwa kutokana na kiwewe ambacho wengi wa watoto hawa wamepitia kabla ya kufika Marekani, huduma ya kisaikolojia pia hutolewa. "Matokeo chanya ya ushirikiano huu kati ya serikali ya shirikisho na Mashirika ya Kikatoliki ya Kutoa Misaada," alisisitiza, "yanaweza kuonekana kwa urahisi katika maisha ya watoto walioishi katika makao ya Pedro Pan ambao, kupitia ushirikiano huu, walikuwa watu wenye mafanikio katika jamii zetu."

Dhamira yake kukuza afya,ustawi na utulivu wa watoto wasio na walezi

Askofu Mkuu aidha alibainisha kuwa "wahitimu" wa Pedro Pan ni pamoja na viongozi wa biashara na wanasiasa, akiwemo seneta wa zamani, wasomi, madaktari, wanasheria, mapadri, na Maaskofu. Askofu Mkuu alikiri kwamba idadi ya watoto wasio na wasaidizi wanaoingia nchini imepungua, na alisema inaeleweka kwamba baadhi ya programu zinaweza kupunguzwa au hata kuondolewa. "Lakini kutokana na historia na sifa ya Kituo cha Askofu Bryan O. Walsh, alisema, "inashangaza kwamba serikali ya Marekani ingefunga programu ambayo itakuwa vigumu kuiga katika kiwango cha uwezo na ubora ambacho Mashirika ya Kikatoliki yamefikia ikiwa na wakati mawimbi ya baadaye ya watoto wasio na walezi yatafika pwani zetu." Askofu Mkuu Wenski alihitimisha taarifa yake akibainisha kuwa Ofisi ya Makazi Mapya ya Wakimbizi, shirika la ndani ya Idara ya Afya na Huduma za Kibinadamu ya Marekani, inajumuisha katika utume wa dhamira yake kuhamasisha afya, ustawi, na utulivu wa watoto wageni wasiosindikizwa. Askofu Mkuu alisema Ofisi ya Makazi Mapya ya Wakimbizi iliahidi kutenda kwa maslahi ya mtoto, ikibainisha kwamba, "Hili pekee linapaswa kuhitaji mapitio ya uamuzi wa kufunga programu hii ya urithi huu."

Imesasishwa tarehe 20 Aprili 2026 saa 6.57 mchana na Angella Rwezaula.

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.

20 Aprili 2026, 12:47