Kelele za vita zinapozimisha sauti ya amani
Na Padre Ibrahim Faltas,OFM.
Huko Yerusalemu, hofu inaonekana imezidi. Mitaa mitupu, sehemu za ibada zisizofikika, na maduka yaliyofungwa ya Jiji la Kale, na waliojeruhiwa na uharibifu katika miji mingi ya nchi Takatifu imekuwa tena mahali ya mateso ya nchi hii iliyouawa kishahidi. Ni makovu yanayoonekana na majeraha yasiyoonekana yanayoonyesha maumivu na kiwewe cha kile kilichotokea na kuzuka upya na mara kwa mara kwa vita visivyo na mwisho. Kuvunja ukimya wa mji ulioachwa ni sauti ya ving'ora, ambavyo husababisha uchungu huku ukisubiri makombora ambayo yataleta vifo na uharibifu zaidi. Hofu ilirudi kwa nguvu, au labda haikuwahi kutoweka kabisa, asubuhi ya Jumamosi kama hiyo ya kusikitisha ya tarehe 7 Oktoba 2023.
Waathiriwa wasio na hatia
Pamoja na walimu na wafanyakazi wa shule, tuliweza kudumisha utulivu uliohitajika ili kuwatuliza watoto huku tukiwasubiri wazazi wao, ambao walikuwa wamewaacha watoto wao kwenye mlango wa shule. Haikuwa rahisi kwa walimu kuzuia machozi yao walipokuwa wakiwatuliza watoto, ambao walikuwa wamesoma pamoja sala rahisi ya Mtakatifu Francis kabla ya kuingia darasani. Niliwatazama watoto, kiwewe kilichofichwa machoni mwao wenye huzuni; nilihisi ufahamu na uwajibikaji wa watu wazima, mateso yao kwa sababu kurudi kwa vurugu kungeleta umbali mpya kutoka kwa utulivu wa kukaribisha wa shule: mawazo haya na wasiwasi huu hujaa akili na moyo wangu. Karibu na Maeneo Matakatifu, tunaishi kawaida inayoonekana kwa sababu tunaamini, tunaomba, na tunatumaini, lakini kelele kubwa ya vita huturudisha kwenye ukweli wenye uchungu kila wakati. Watoto hawaelewi vurugu; hawajui sababu zisizo za kibinadamu za vurugu, na wanaendelea kuwa waathiriwa wasio na hatia wa upuuzi wa uovu. Watoto wanaelewa na kutambua wema pekee. Katika nyakati hizi wanatetemeka, na ni uovu unaowafanya watetemeke; ni hofu ya kitu wasichokijua inayoondoa tabasamu ya watoto wote wanaoteseka na kufa katika nchi ambazo ni mandhari ya vita. Wanakufa na kuteseka huko Gaza, Tehran, Kyiv, Tel Aviv. Wanaogopa, wana huzuni, wanateseka kwa njaa na baridi, wanaogopa chini ya makazi ya mahema yenye unyevunyevu, wametengwa katika giza la makazi na mabanda, wamezikwa chini ya vifusi vya shule na nyumba, hawachezi, na hawatumii kalamu na penseli za rangi.
Hili ni matokeo yasiyo ya kibinadamu ya vita
Baada ya tarehe 7 Oktoba 2023, kulikuwa na wito na maombi mengi kwa jumuiya ya kimataifa ili kuwa binadamu tena. Mapapa wawili waliomba amani kwa nguvu kubwa, kama vile mamlaka za kiraia na kidini, wanaume na wanawake wa kawaida, na watu mashuhuri. Majibu hayajapatikana, na kama yamepatikana, hadi sasa hayajatoa matokeo wala suluhisho lolote huko Gaza, katika Nchi Takatifu, na katika maeneo mengine yaliyokumbwa na miaka mingi ya vita na vurugu. Ni nani aliyepaswa kujibu maombi ya amani? Ni ubinadamu gani unaowajibu wanadamu waliojeruhiwa? Haya ni maswali ambayo hayawezi kupata majibu ikiwa, kwa miaka mingi, haki muhimu za wasio na hatia zinaendelea kukanyagwa, na ikiwa majukumu ya jumuiya ya kimataifa yanasimamiwa kulingana na maslahi ya uchumi wa vita na kwa kutojali wale wanaoteseka. Huko Gaza, watoto walionyimwa haki ya utulivu, badala ya kupokea msaada na elimu, wanalazimika kutafuta vitu ambavyo wanaweza kuuza tena kwenye kifusi badala ya chakula na blanketi. Ni ubinadamu gani unaowaunga mkono na kuwasaidia wanapochimba vumbi na kumbukumbu za wasio na hatia wengine? Ni nani bado anawakumbuka? Ni ubinadamu gani ambao hauruhusu msaada kuwafikia wale waliokuwa wakitafuta usalama na kupoteza maisha yao baharini, ambayo sasa inarudisha kwenye miili na ndoto za matumaini? Ni ubinadamu gani ambao hauheshimu wakati na masharti ya makubaliano ambayo yanaweza kuwapa nafasi ya kupumzika na kupumua wale wanaosubiri mwisho wa vurugu na mateso yasiyofikirika?
Maswali yasiyo na majibu
Haya ni maswali ambayo hatuna majibu yake, maswali ambayo ubinadamu wa wale ambao, kama Papa Leo XIV asemavyo, wana jukumu la kimaadili la kuzuia uovu kuwa mhusika mkuu wa nyakati zetu hawajibu. Uzoefu wangu katika Nchi Takatifu bado unaniongoza kuamini na kutumaini katika mioyo ya wanadamu wanaowapenda jirani zao bila mawazo ya awali na bila mipaka, ambao hutoa mkono wa kirafiki, kusikiliza kwa makini, kukumbatiana kunakotia joto roho. Huu ni ubinadamu ambao kila mwanadamu anapaswa kujitambua; huu ndio ubinadamu ambao jumuiya ya kimataifa lazima iwakilishe. Haki na wajibu, wajibu na heshima ni vipengele muhimu vya kubaki binadamu, kuamini, kuwa na imani na matumaini katika ubinadamu, na kuondoa mlio vita na kutoa sauti kwa sauti ya amani.
Asante kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here