Baraza la Maaskofu Nchini Sierra Leone. Baraza la Maaskofu Nchini Sierra Leone. 

Sierra Leone:Maaskofu walaani ongezeko la vurugu dhidi ya Mapadre

Maaskofu Katoliki nchini Sierra Leone walielezea wasiwasi wao kuhusu vitendo visivyokubalika na kulaani ongezeko la mashambulizi ya vurugu yanayowalenga Mapadre, Watawa na mali za Kanisa kote nchini.

Na Sr. Christine Masivo, CPS – Vatican.

Maaskofu Katoliki nchini Siera Leone walitoa taarifa na kuonesha wasiwasi wao kuhusu vitendo visivyokubalika vya kuongezeko la mashambulizi dhidi ya wafanyakazi wa Kanisa na taasisi zake  na kulaani ongezeko hilo la vurugu  yanayowalenga Mapadre, Watawa na mali za Kanisa kote nchini. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirika la Kipapa la Habari za Kimisionari FIDES, linabinisha kwamba shambulio la hivi karibuni la Padre walibainisha kuwa "Sisi, Maaskofu Wakatoliki nchini Sierra Leone, tunalaani vikali na kushutumu mashambulizi dhidi ya mapadre, Watawa na uporaji wa mali za Kanisa katika majimbo yetu."

Mashambulizi 27 Januari 2025 na 30 Agosti 2025

Mnamo tarehe 27 Januari 2025, tukio la hivi karibuni Padre James Joshua Jamuri, wa Parokia ya Kupalizwa Bikira Maria huko Pendembu, Upper Bambara, alishambuliwa na kujeruhiwa kwenye mkono wake kichwani na magotini. Mshambuliaji huyo alikamatwa na yuko chini ya ulinzi wa polisi. Maaskofu pia walikumbuka mauaji ya kikatili ya Padre Augustine Dauda Amadu wa Parokia ya Maria Mkingiwa Dhambi huko Kenema ambaye aliuawa usiku wa  tarehe 30 Agosti 2025, walielezea mshikamano wao mkubwa na wasiwasi kwa waathiriwa kwenye mashambulizi haya ya mara kwa mara. Padre Amadu alishambuliwa nyumbani kwake, na kuacha Jumuiya ya Wakatoliki nchini kote wakiwa wameshtuka. Uchunguzi umefanywa na hadi sasa watu sita wamekamatwa kufuatia mauaji ya Padre Amadu. Mshtakiwa aliiba Kompyuta ya mkononi yenye thamani ya dola 350 na pesa taslimu 5,000 za Sierra Leone Leone.

Mshikamano usioyumba wa Maaskofu kwa Jumuiya

Maaskofu walibainisha kuwa miezi sita baada ya mauaji ya Padre Chinedu na matokeo ya Padre Jamiru, wizi umeongezeka kulenga vituo vya misheni na mali za Kanisa. Hii imesababisha kunyimwa jamii hasa walio katika mazingira magumu na maskini huduma muhimu. Wakithibitisha tena "mshikamano wao usioyumba na mapadre, watawa na waamini ambao wameumizwa na mavazi ya kijeshi, uvamizi wa makazi yao na uporaji wa mali za misheni," maaskofu walitangaza kwamba "hii inatosha!" Taarifa hiyo ilihitimishwa kwa wito mkubwa kwa mamlaka za kutekeleza sheria na polisi kuchukua hatua madhubuti kuzuia vurugu zaidi na kuhakikisha usalama wa mapadre, jumuiya za kidini, na taasisi za kanisa kote Siera Leone.

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku: Just click here

 

06 Februari 2026, 14:32